• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Zaidi ya Shilingi Milioni 30 Kushindaniwa Simiyu Jambo Festival 2019

Posted on: June 25th, 2019

Tamasha kubwa la michezo ambalo hufanyika kila mwaka Mkoani Simiyu (Simiyu Jambo Festival) linatarajiwa kufanyika Juni 30, mwaka huu katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi huku takribani shilingi milioni 32 zikishindaniwa.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Juni 25, Mratibu wa tamasha hilo Bi. Zena Mchujuko amesema Mgeni rasmi katika Tamasha hili anatarajiwa kuwa Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson.

Amesema katika Tamasha hilo kutafanyika mashindano ya mbio za baiskeli wanaume na wanawake, mbio fupi kilometa tano wanaume na wanawake na mashindano ya mdahalo kwa wanafunzi wa shule za sekondari.

“Jumla ya shilingi milioni 32 zitashindaniwa kwa michezo yote,  mshindi wa kwanza mbio za baiskeli kwa wanaume atapata 1,000,000, Wanawake 700, 000, walemavu 500, 000 na tutatoa zawadi mpaka kwa mshindi wa 25;  ngoma za asili mshindi atapata 1,000,000” alisema Bi. Zena

Aidha, amesema fomu za ushiriki zinapatikana kataika ofisi ya Chama cha Baiskeli Mkoa wa Simiyu Mjini Bariadi na katika Tovuti: www.simiyutalent.co.tz kwa gharama za shilingi elfu tano(5000) kwa mashindano ya baiskeli na shilingi elfu mbili (2000) kwa ajili ya mashindano ya mbio fupi.

Katika hatua nyingine Bi. Mchujuko amesema kupitia Tamasha la Simiyu Jambo Festival jamii ya watu wa Simiyu itapata ujumbe wa kupinga mimba za utotoni jambo litakalopelekea watoto wa kike waweze kutimiza ndoto zao kupitia Kauli Mbiu ya Tamasha ambayo ni :-WEZESHA MTOTO WA KIKE ATIMIZE NDOTO ZAKE, INAWEZEKANA KUZUIA MIMBA KATIKA UMRI MDOGO”

 

Mratibu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu Duniani(UNFPA) Mkoa wa Simiyu, Dkt. Amir Batenga amesema shirika hilo limekuwa likishirikiana na Serikali katika jitihada za kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi, ambapo waathirika wakubwa ni wasichana wenye umri mdogo, hivyo anaamini kupitia Tamasha hilo wananchi watapata ujumbe mahususi wa kukabiliana na mimba katika umri mdogo.

Naye Katibu wa Chama cha Mbio za Baiskeli Mkoa wa Simiyu, Bw, Samwel Richard washiriki takribani 260 kutoka mikoa ya Simiyu, Shinyanga, Mara, Mwanza, Geita na Kagera wanatarajia kushirikia mashindano ya baiskeli, huku akiwahakikishia wananchi kuwa wachezaji wao wamejiandaa vizuri na wamekuwa kambi kwa takribani wiki mbili.

Kwa upande wake Kiongozi wa Ngoma za Asili Mkoa wa Simiyu, Bw. Buhimila Shala amesema kupitia ngoma za wagika na wagalu watatoa ujumbe uliobebwa na Kauli mbiu ya Tamasha kwa lengo la kuwaokoa wasichana kupata mimba katika umri mdogo.

Tamasha la Simiyu Festival mwaka 2019 limedhaminiwa na Jambo Food Products Company, Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani-UNFPA, NGM Gold Mine Limited, NGS Petroleum, Alliance Ginneries Limited, Busega Mazao Limited, Maswa Standard Chalk, Ms Hotel na Vetreces Company Limited.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/06/zaidi-ya-shilingi-milioni-30.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa