• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Waziri wa Kilimo Prof. Mkenda, Naibu Waziri TAMISEMI Dkt Dugange Wanogesha RCC Simiyu

Posted on: December 16th, 2020

Waziri wa Kilimo, Profesa Adolf Mkenda na Naibu  Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Dkt. Festo Dugange wameshiriki kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Simiyu (RCC), ambapo walitumia fursa hiyo kuwasilisha masuala ya kilimo na afya kwa viongozi wa chama na serikali, wakuu wa Taasisi za Umma na binafsi, viongozi wa Dini na wadau wengine wa maendeleo.

Akizungumzia kuhusu kilimo cha zao la pamba katika kikao hicho kilichofanyika Desemba 15, 2020 Mjini Bariadi Prof. Adolf Mkenda amesema Wizara ya kilimo itafanya mapitio ya  mifumo mbalimbali ya kitaasisi ili kuongeza tija katika  uzalishaji wa pamba kufikia lengo la kuzalisha tani milioni moja ndani ya miaka mitano ijayo.

Miongoni mwa mifumo aliyoibainisha Profesa Mkenda ni pamoja na mfumo wa kushughulikia pembejeo za kilimo huku akibainisha kuwa Wizara yake  inaendelea kufanya uchunguzi ili kuona kama uwezekano wa kuzalisha viuatilifu  nchini ili kupunguza uagizaji wa viuatilifu kutoka nje ya nchi na kuweza kudhibiti ubora wa viuatilifu hivyo.

“ Katika kufikia tija kwenye zao la pamba pia tunapitia upya na kwa haraka sana mfumo mzima wa kitaasisi wa kuzalisha na kugawa mbegu za pamba, utaratibu mpya hautakuwa umekamilika kwa kipindi hiki cha msimu huu, lakini tumekusudia na tumekubaliana tutafanya mapitio ili wakulima wapate mbegu bora kwa wakati,” alisema Profesa Mkenda.

Awali Kabla ya kuzungumza katika  kikao hicho Prof. Mkenda, wajumbe wa Kikao cha RCC waliwasilisha changamoto mbalimbali katika kilimo cha pamba ikiwa ni pamoja na tatizo la upungufu wa mbegu na mbegu kutowafikia wananchi kwa wakati.

“Kumekuwa na changamoto ya upungufu wa mbegu kwa wakulima, ninashauri ili mbegu ziwafikie wakulima wote na kwa wakati, makampuni yanayozalisha mbegu yazipeleke kwa Mkurugenzi ambaye ndiye mwenye wataalam wa kilimo wanaofahamu idadi ya wakulima na ukubwa wa maeneo wanayolima,” alisema Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Benson Kilangi.

“Pamoja na kutatua changamoto ya pamba, tunaomba serikali iajiri maafisa ugani  ili wananchi waweze kupata huduma za ugani na kuzalisha kwa tija,tutakapozalisha kwa tija tutapata mavuno mengi na mkulima atanufaika pamba yake, suluhisho la bei ya pamba ni kujenga kiwanda cha nguo mkoani Simiyu,” Mhe. Esther Midimu Mbunge Viti Maalum.

Kwa upande wake Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEMI Dkt. Festo Dugange ametoa rai kwa Wakurugenzi wa Halmashauri za Wilaya ya Busega, Bariadi na Itilima kuanza kununua vifaa tiba kwenye Hospitali za Wilaya zilizojengwa kwa kutumia mapato ya ndani  huku akibainisha kuwa Serikali imetenga shilingi milioni 500 kwa kila hospitali kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba.

Dkt. Dugange pia amesema katika miaka mitano ijayo Serikali ina mpango wa kujenga vituo vya kutolea huduma za afya takribani 655 huku akifafanua kuwa itaanza na ukamilishaji wa maboma yaliyojengwa na kwa nguvu za wananchi na kuomba Halmashauri kuweka mpango wa kuanza kukamilisha maboma hayo.

Dkt.Dugange amesisitiza juu ya umuhimu wa kuimarisha usimamizi wa mifumo ya ukusanyaji mapato  katika vituo vya kutolea huduma za afya, ambapo amebainisha kuwa makusanyo yakiwa mazuri yatazipunguzia Halmashauri mzigo wa utegemezi kwa Serikali Kuu na wadau mbalimbali wa afya na kuwezesha vituo hivyo kujiendesha ikiwa ni pamoja na kuwa na uwezo wa kununua dawa.

Akifunga kikao cha RRC Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewashukuru viongozi hao kushiriki katika kikao hicho, huku akitoa wito kwa viongozi wote wa Mkoa huo kuifanya elimu kuwa ajenda ya kudumu ya mkoa na ujenzi wa vyumba vya madarasa kuwa ni kipaumbele chao cha kwanza ili kila mwanafunzi aliyefaulu aweze kwenda shule.

MWISHO.

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/12/waziri-wa-kilimo-prof-mkenda-naibu.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa