• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Waziri wa Kilimo Azindua Bima ya Mazao

Posted on: August 3rd, 2019

Serikali kupitia waziri wa kilimo Japhet Hasunga imezindua Bima ya Kilimo inayokinga mazao ya mkulima yanapokuwa shambani dhidi ya ukame, magonjwa ,wadudu waharibifu , mvua zilizozidi, moto, uharibifu unaoweza kusababishwa na wanyapori, pamoja na mvua ya mawe.

Akizundua bima hiyo Hasunga amesema kuwa wameamua kuanza na kipaumbele katika zao la pamba ambalo huzalishwa kwa wingi Mkoani hapa lengo likiwa ni kuwainua wakulima wenye vipato vya chini sambamba na kuwasaidia kupata msaada pindi wanapopatwa na majanga ambapo bima hiyo inatarajiwa kuzinduliwa kwenye mazao mengine ya kimkakati.

Aidha waziri Hasunga amewataka wakulima walio katika vyama vya msingi vya ushirika (AMCOS) kuhakikisha wanajiunga na bima ya mazao itakayowasaidia kukuza uchumi wao na kuongeza kuwa idadi ya vyama vya ushirika katika mazao yote imeongezeka na kufikia 11,331 ambapo kiwango cha ukaguzi wa vyama hivyo ni 70% na kuisisitiza Tume ya Maendeleo ya Ushirika kuongeza kasi ya ukaguzi ili ifikie 100%.

“Bima hiyo ya mazao itamsadia mkulima kuepukana na majanga mbalimbali na kwamba tumeamua kulipa kipaumbele zao la pamba na baada ya hapa tutaenda Kagera kuzindua bima kwenye zao la kahawa na serikali imelenga kuongeza kuwainua wakulima ili waweze kuchangia katika kukuza pato la Taifa”alisema waziri Hasunga

Ameongeza kuwa wakati umefika wa kuwachukulia hatua za kisheria waliohujumu vyama vya ushirika awali huku akiwataka waliopewa majukumu kwenye AMCOS kuwa wachapakazi, waadilifu na waaminifu katika utendaji kazi wao.

“nitoe tamko kuwa viongozi wote wa vyama vya ushirika ambao wanawafanya ubadhilifu na kuihujumu serikali ni lazima wachukuliwe hatua za kisheria na pia ni vyema sasa sheria na miongozo iliyopo ibadilishwe ili iweze kuendana na kasi ya ushirika uliopo” alisema

Awali Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima ya Taifa (NIC) dokta Elirehema Doriye amesema kuwa shirika hilo linatarajia kutoa bima ya mazao kwa wakulima wote nchini huku akiwashauri wakulima kukata bima ili kuepukana na changamoto.

Aidha ameongeza kuwa bima hiyo itamsaidia mkulima kuweza kukopesheka kwenye mabenki kwani tayari mkulima atakuwa na kinga hivyo kutoa mazao yatakayochangia pato lake na Taifa kwa ujumla huku akiongeza kuwa shirika hilo linalomilikiwa na serikali kwa asilimia mia moja 100% likiwafikia wakulima wote na kwa kuanzia wataanza na wakulima wadogo.

Pamoja na hayo ameongeza kuwa bima hiyo ina manufaa makubwa kwa mkulima na itamkomboa kutoka katika kilimo kidogo na kwenda kikubwa kitakachomuwezesha kuwekeza katika kilimo cha kisasa bila kuwa na hofu ya kupoteza mtaji aliowekeza shambani ikiwa sekta kilimo imeajiri zaidi ya 75% ya Watanzania.

Kwa upande wake Kamishina wa Bima hapa nchini Dkt. Mussa Juma ameeleza kuwa lengo la bima hiyo ni kusaidia kuinua kipato cha watu wenye kipato cha chini ili waweze kuchangia katika ukuzaji wa uchumi wa nchi .

Mbali na hayo amesema kuwa uchumi wa nchi unategemea sekta mbalimbali ambazo ni kama kilimo, uvuvi, mifugo, madini na ili kuwa na viwanda ambavyo vinaweza kusaidia kukuza uchumi wa nchi lazma kuwe na namna ya kudhibiti majanga.

Hata hivyo ameongeza kuwa bima ambazo zinahusu watu wengi hasa wenye kipato cha chini mamlaka imeona iweze kuwafikia kwa namna moja nyingine.

Awali akimkaribisha waziri Hasunga mkuu wa mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka amesema kuwa mkoa umejiandaa kikamilifu kusaidiana na NIC katika kuhakikisha zaidi ya wakulima 100,000 wa pamba waliosajiliwa wanapata bima ya mazao.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI  FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/08/waziri-hasunga-azindua-bima-ya-mazao.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa