• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wazazi, Walezi Wapunguzieni Kazi Wanafunzi wa Madarasa Ya Mitihani: RC Mtaka

Posted on: October 9th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa wazazi na walezi kuwapunguzia kazi wanafunzi walio katika madarasa ya mitihani ya Taifa (darasa la nne, kidato cha pili na kidato cha nne) ambayo inatarajiwa kufanyika hivi karibuni ili waweze kujipatia muda mwingi wa kujisomea kujiandaa na mitihani hiyo.

Mtaka ameyasema hayo jana wakati makabidhiano ya Chuo cha Ufundi Kasoli katika Kijiji cha Kasoli wilayani Bariadi kilichojengwa na mwekezaji Alliance Ginnery Limited na kukabidhiwa kwa Serikali na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Dkt. Maduhu Kazi kwa niaba ya kampuni hiyo na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa niaba ya wananchi.

“Darasa la saba wameshafanya mtihani wao, watoto wa darasa la nne, kidato cha pili na kidato cha nne waendelee kufanya maandalizi, wazazi na walezi wapunguzieni kazi watoto wote walio kwenye madarasa haya na wakiwa nyumbani wafanye majadiliano ya pamoja,” alisema Mtaka.

Aidha, Mtaka amewaonya wazazi na walezi wenye nia ya kuwaozesha wanafunzi wa kike waliohitimu elimu ya msingi kuwa watakaofanya hivyo watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria, huku akitoa wito kwa jamii yote kuwa walinzi wa watoto wa kike ili waweze kutimiza ndoto zao.

Mtaka ameishukuru Kampuni ya Allience Ginnery kujenga chuo cha ufundi Kasoli na kutoa wito kwa wasichana na wanawake kijiji cha Kasoli kujitokeza kupata mafunzo ya ushonaji bila malipo katika chuo hicho katika kipindi cha mwezi Oktoba hadi Desemba, kabla ya kuanza kwa mafunzo yatakayoanza mwakani kwa mtaala wa Serikali na kuahidi kutoa vyerehani 25.

Meneja Mkuu wa Alliance Ginnery Limited, Bw. Boaz Ogola amesema Kampuni hiyo imekuwa inajihusisha sana na maendeleo ya jamii katika sekta ya elimu, afya na maji kwa kuwa wao ni sehemu ya jamii, ni wajibu wao kufanya hivyo na ni sehemu ya maelekezo ya TIC wanayopewa wawekezaji wote.

“Tunashiriki kwenye masuala ya jamii kwa sababu sisi ni sehemu ya jamii, sisi tunashughulika na wakulima na wanaotulimia pamba na kutuuzia kutuwezesha kuendesha kiwanda chetu, siku za nyuma tulijikita kwenye afya, maji na elimu ya msingi na sekondari; tumeona haja ya kujenga chuo cha ufundi ili wanafunzi watakaoshindwa kuendelea na masomo, wapate mafunzo ya ufundi ili waweze kujitegemea,” alisema Ogola.

Aidha, Ogola amesema pamoja na mafunzo ya ufundi mipango ya baadaye ya kampuni ya Alliance Ginnery kuongeza darasa moja la wakulima kwa lengo la kutoa warsha na mafunzo kwa wakulima ili waweze kulima kilimo chenye tija ili kampuni hiyo iweze kupata malighafi bora kwa ajili ya kiwanda chake cha kuchambua pamba..

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Dkt. Maduhu Kazi ameipongeza na kuishukuru Kampuni ya Alliance Ginnery kujenga chuo cha Ufundi na kutoa wito kwa wawekezaji wengine kuona umuhimu wa kuwafikia wananchi walio katika maeneo yao huku akiahidi kuwa TIC itahakikisha kinakuwa mstari wa mbele kutatua changamoto zinazowakabili wawekezaji.

“TIC inashirikiana na Serikali hata ngazi ya mikoa na tumejielekeza zaidi kuongeza ufanisi katika shughuli zetu za kuwasaidia wawekezaji masuala ya vibali kwa kushirikiana na Taasisi zinazohusika; pia tumejipanga hata kuwafikia wawekezaji wadogo Watanzania maana baada ya tathmini tumeona eneo hilo kuna mapungufu maana wengi wanadhani sisi tunahusika na wawekezaji wa kigeni tu,” alisema Dkt. Kazi.

Naye Mkazi wa Kijiji cha Kasoli Shamsa Abdallah amesema anaishukuru Kampuni ya Alliance Ginnery kwa kuwajengea chuo cha ufundi na anaamini kuwa kitawasadia kwenye mafunzo ya ushonaji na mafunzo yanayohusiana na kilimo yatakayowasaidia kujikwamua kiuchumi.

Kampuni ya Alliance Ginnery Limited imejenga majengo ya chuo cha ufundi Kasoli kwa gharama ya zaidi ya shilingi milioni 180, kuchimba kisima cha maji chenye uwezo wa kutoa lita 5000 kwa saa pamoja na kuweka vifaa kama vyerehani, majiko ya gesi na vifaa mbalimbali vya kujifunzia upishi,vifaa vya kujifunzia uashi na useremala meza na viti vya ofisi.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI TEMBELEA BLOGU YA MKOA KUPITIA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/10/wazazi-walezi-wapunguzieni-kazi.html


Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa