• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wazazi Waaswa Kuwalea Watoto Katika Maadili Mema, Kuwaepusha na Dawa za kulevya, Maambukizi ya VVU

Posted on: September 19th, 2018

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera ,Bunge Kazi,Vijana ,Ajira na Walemavu  Mhe. Anthony Mavunde ametoa wito kwa Wazazi nchini kuwalea watoto wao katika maadili mema ili kuwaepusha na matumizi ya dawa za kulevya na Maambukizi ya   Virusi Vya Ukimwi.

Ushauri huo ameutoa wakati akifungua makambi ya siku saba ya Kanisa la Waadventisa Wasabato mkoani SIMIYU, katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi.

Mavunde amesema malezi ya watoto ni jambo muhimu sana hasa katika kizazi cha hivyo watoto wakikosa malezi bora katika umri walio nao ni rahisi kutumbukia katika makundi yasiyofaa yakiwemo ya matumizi ya dawa za kulevya na hivyo kukosa nguvu kazi ya Taifa.

“Kwa mujibu wa takwimu Tanzani kila siku watu 200 wanapat maambukizi mapya ya VVU katika watu 200 watu 80 ni vijana katika hao vijana 80 asilimia 80 ni watoto wa kike, hivyo tuendelee kuelemisha  na kuliandaa hili kundi kubwa la Vijana katika malezi bora ili wawe nguvu kazi ya kuleta tija katika Taifa letu” alisema.

Ameongeza kuwa ili watu waweze kuondokana na umaskini ni lazima wafanye kazi hivyo akatoa wito kwa Viongozi, waumini wa Kanisa la Waadventisa Wasabato na wananchi wote kufanya kazi kwa staha, uadilifu na malengo ili waweze kufanikiwa kiuchumi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema makambi hayo ni sehemu ya Maandalizi ya Mkutano mkubwa wa Chama cha Wanataaluma na Wajasiriamali Waadventista Wasabato (ATAPE) unatarajiwa kufanyika mwaka 2019 mkoani humo.

Aidha, Mtaka alitumia fursa hiyo kuwaeleza wananchi kuwa mwaka 2019 kutakuwa na matukio makubwa matatu ambayo yataitambulisha Simiyu ambayo ni mkutano huo wa ATAPE, Mkutano wa Madaktari wa Nchi nzima na Maonesho ya Nanenane ya Kimataifa.

Katika hatua nyingine amewahimiza wananchi kujifunza masuala ya Ujasiriamali na kuwakaribisha katika Maonesho ya Viwanda Vidogo SIDO yatakayofanyika Kitaifa mwaka huu 2018 kuanzia tarehe 24 hadi 28 Oktoba, 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi.

Awali akitoa somo kuhusu masuala ya Ujasiriamali, Mchungaji Joshua Njuguna aliwasisitiza waumini wote kuwa siyo mpango wa Mungu mtu yeyote awe maskini , akawaasa kufanya kazi ili kuutafuta utajiri  hivyo akawataka wazitafute fursa za kupata utajiri  na kufanya kazi kwa bidii.

Pia Naibu Waziri Mavunde ameahidi kuchangia jumla ya mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya kuwaunga mkono Waumini hao katika ujenzi wa Hospitali ya Kanisa katika eneo la Pasiasi jijini Mwanza.

Ufunguzi wa makambi umehudhuriwa na waumini mbalimbali kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini, lengo likiwa ni kujifunza neno la Mungu, kutoa elimu ya ujasiriamali, mafunzo ya ndoa na malezi ya watoto na  kuliombea Taifa.

MWISHO

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa