• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wazawa Watakiwa kupewa Kipaumbele Maeneo ya Uwekezaji wa Viwanda

Posted on: July 9th, 2017

Halmashauri ya wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu imetakiwa kutoa kipaumbele kwa wawekezaji wazawa pindi wanapogawa maeneo ya uwekezaji wa viwanda ili kusaidia kukuza ajira na uchumi ndani na nje ya Mkoa, ambapo jumla ya ekari 1000 zimeshatengwa kwa ajili yauwekezaji.

 Wito huo umetolewa leo na Kiongozi wa  Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa mwaka 2017 Amour Hamad Amour wakati wa kukagua na kukabidhi hati ya eneo la uwekezaji wa viwanda kwa Mkurugenzi wa  Halmashauri  lililopo katika kata ya Nyalikungu Wilaya ya Maswa
 .
Kiongozi huyo amepongeza Uongozi wa Wilaya ya Maswa kwa kutekeleza agizo la Serikali la kutenga eneo la uwekezaji na kusema kuwa ni vema wazawa wakapewa kipaumbele kwa kupatiwa maeneo hayo, ili waanze ujenzi wa viwanda mbalimbali vitakavyokuza ajira, kuchangia pato la Halmashauri, pato la mwananchi mmoja mmoja  na uchumi wa Nchi kwa ujumla.

 "Nashauri Halmashauri kutoa kipaumbele kwa wazawa kwa kuwapatia maeneo hayo ya viwanda ili wafanye shughuli za kimaendeleo ambazo zitagusa moja kwa moja maisha ya Wananchi wa Wilaya ya Maswa, mkoa wa Simiyu na Taifa kwa ujumla ikiwa ni pamoja suala la ajira kwa vijana ....Alisema.

Pamoja na kuwapa kipaumbele wazawa Ndg. Amour ameutaka uongozi wa Wilaya ya Maswa kutoa ushirikiano kwa wawekezaji wageni na kutoa maeneo kwa wote watakaokidhi masharti ya kuwekeza na kujenga viwanda  kwa mujibu wa sheria za nchi.


Aidha Amour ameishauri Halmashauri hiyo kuanzishwa viwanda ambavyo vitayaongezea thamani mazao na kutoa bidhaa zitakazoingia sokoni moja kwa moja,  badala ya kung'ang'ana viwanda vinavyoandaa malighafi zitakazotumiwa na viwanda vilivyo nje ya nchi; kama ilivyo kwa viwana vingi vya pamba huandaa pamba inayoenda kuzalisha nguo nje ya nchi.

 Pia amefurahishwa na kuupongeza uongozi  mzima wa Halmashauri hiyo kwa jitihada wanazozifanya za kuanzisha viwanda vinavyoiongezea halmashauri mapato kikiwemo kiwanda cha Chaki, sambamba na kuhakikisha wanaendana na kasi ya Mhe Rais ya kuwa na Tanzania ya viwanda .

Naye Afisa Mipango Miji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa John Nkoko amesema kuwa tayari wameshatenga ekari 1000 kwa ajiri ya eneo la viwanda na tayari eneo la ekari 315.64 limeshaandaliwa michoro ya mipango miji.

Nkoko amesema kuwa lengo la Halmashauri yao kutenga eneo hilo ni kuhakikisha wanatengeneza fursa ya ajira kwa wananchi wao pamoja na kukuza uchumi wao wa ndani na nje ya Mkoa .

 Sambamba na hilo Mkurugenzi wa Halmashauri ya Maswa Dk Fredrick Sagamiko alisema Wilaya yake itahakikisha inapambana kuwa na uchumi wa kati kwa kuanzisha viwanda mbalimbali ambapo mpaka sasa wameanza ujenzi mpya wa kiwanda kikubwa cha chaki ambacho kitakuwa cha kwanza Afrika Mashariki kwa kuwa na teknolojia mpya.

Mwenge wa Uhuru ukiwa Wilayani Maswa umeweka mawe ya mingi, kuzindua, kufungua na kuona miradi mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya Viwanda, Afya, Elimu, Kilimo, Utawala Bora,Maendeleo ya Jamii,Ardhi Maliasili na Mazingira.

Akitoa Ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru katika maeneo mbalimbali ya miradi Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru amewaasa wananchi kufanya kazi kwa bidii, kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli katika kulinda rasilimali za nchi pamoja na kupambana na rushwa, dawa za kulevya, malaria na UKIMWI.

  


Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa