• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Watu Wenye Ulemavu Watakiwa Kuchangamkia Fursa ya Mikopo ya Asilimia Mbili Kutoka Halmashauri

Posted on: January 30th, 2021

Na Stella Kalinga, Simiyu RS

Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya watu wenye Ulemavu, Mhe.Ummy Nderiananga amewataka watu wenye ulemavu nchini kujitokeza kuchukua mikopo inayotolewa na halmashauri bila riba kutoka katika asilimia mbili ya mapato ya ndani ili waweze kujipatia kipato na kuondokana na adha ya kutumikishwa kama omba omba.

Mhe. Nderiananga ametoa wito huo jana Januari 29, Mjini Bariadi wakati alipokutana na kuzungumza na viongozi wa makundi mbalimbali ya watu wenye ulemavu akiwa katika ziara yake ya siku moja mkoani Simiyu, iliyolenga kufanya ufuatiliaji na uhamasishaji wa masuala ya watu wenye ulemavu..

" Licha ya baadhi ya Halmashauri kufanya vizuri katika kutenga fedha kwa ajili ya watu wenye ulemavu, kuna taarifa kuwa baadhi yenu mmekuwa waoga kukopa fedha zinazotengwa kwa ajili yenu, nitoe rai kwenu tumieni fursa hiyo kopeni ili mpate mitaji ya kuwasaidia kufanya shughuli za kuwaingizia kipato, fedha hizi ni kwa ajili yenu na Serikali imefanya kazi kubwa sana ili mpate fedha hizi,” alisema Nderiananga.

Katika hatua nyingine Nderiananga amewaasa watu wenye ulemavu wanaochukua mikopo hiyo kurejesha kwa wakati kwa mujibu wa miongozo na taratibu za utoaji wa mikopo hiyo ili kutoa fursa kwa kila mmoja anayehitaji  mikopo hiyo kuipata kwa wakati.

“Natoa wito kwa watu wenye ulemavu ambao mmekuwa mkikopeshwa fedha itokanayo na asilimia mbili ya mapato ya ndani ya halmashauri kurejesha nawaomba msile, mkila mtafanya watu wenye ulemavu wasiaminike,” alisema Nderiananga

Mwenyekiti wa Chama cha Walemavu wa viungo (CHAWATA) Mkoa wa Simiyu, Bw Gera Makasi ameomba Viongozi na wataalam kutoka Serikalini waendelee kutoa elimu juu ya mikopo hiyo ili watu wenye ulemavu wapate uelewa mpana juu ya namna mikopo hiyo inavyotolewa, inavyorejeshwa na namna sahihi ya kuitumia kwa manufaa.

Naye  Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga amesema Mkoa wa Simiyu unawajali sana watu wenye ulemavu  huku akibainisha kuwa Simiyu imejipanga kuanzisha namna ya tofauti (unique model) ya utoaji wa mikopo kwa watu wenye ulemavu, wanawake na vijana ili mikopo itolewayo kutoka katika asilimia kumi ya mapato ya Halmashauri iwe na tija kwa makundi lengwa ( watu wenye ulemavu asilimia mbili, vijana asilimia nne na wanawake asilimia nne)

Akitoa taarifa ya mkoa kwa Naibu Waziri, Kaimu Katibu Tawala wa mkoa wa Simiyu, Bw. Ekwabi Mujungu amesema watu wenye uemavu mkoani hapa wamekuwa wakishirikishwa katika shughuli za kijamii na uhamasishaji unaendelea kufanyika ili waweze kuunda vikundi kurahisisha upatikanaji wa mikopo, ambapo  mpaka sasa takribani vikundi 45 vya watu wenye ulemavu vimeshaundwa.

Aidha , Mujungu ameongeza kuwa katika bajeti ya mwaka 2020/2021  kiasi cha shilingi milioni mia mbili na laki sita kimetengwa katika halmashauri zote sita za mkoa wa Simiyu (Bariadi Mjini, Bariadi Vijijini, Busega, Itilima, Maswa na Meatu) kwa ajili ya kutoa mikopo kwa watu wenye ulemavu.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2021/01/watu-wenye-ulemavu-watakiwa.html


Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa