• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wanufaika wa TASAF Wahimizwa Kuwapeleka Watoto Shule na Kliniki

Posted on: May 24th, 2017

Wanufaika wa Mradi wa Mpango wa Kunusuru kaya maskini TASAF III hususani wanaopewa ruzuku ya utimizaji wa masharti ya elimu na afya wamehimizwa kuwapeleka watoto kliniki na kuhakikisha watoto wao wanahudhuria shuleni.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Ndani kutoka TASAF Makao Makuu, Ndg. Christopher Sanga katika kijiji cha Migato wilayani Itilima wakati wa ziara ya tathmini ya utekelezaji mradi wa TASAF wilayani humo.

Sanga amesema Serikali ina mpango mzuri kwa wananchi wa kuhakikisha watoto wote wenye umri wa kwenda shule wanapelekwa shule na pia watoto wote wenye umri chini ya miaka mitano wanapelekwa kiliniki na kupata  huduma za afya zinazotakiwa, hivyo akawaasa kutorudisha nyuma juhudi za Serikali.

Aidha, amesema lengo kuu la Serikali ni kuhakikisha nguvu kazi inajengwa kwa kutoa elimu na kuangalia afya za watoto wakiwa bado wadogo ili watakapobainika kuwa na matatizo ya kiafya wapatiwe matibabu mapema kwa lengo la kuimarisha afya na  kutoathiri ukuaji wao.

Ameongeza kuwa utafiti uliofanyika kuhusu utekelezaji wa awamu zilizotangulia za Mpango wa TASAF ulionesha kuwa, kumekuwa na miundombinu mingi ya elimu na afya lakini kaya maskini zimekuwa hazipeleki watoto katika huduma hizo, hivyo Serikali ikatoa ruzuku ya elimu na afya na kuwawekea masharti wazazi ili kuhakikisha wanawapeleka watoto katika huduma hizo.

Amesisitiza kuwa Mpango wa TASAF unafuatilia mahudhurio ya watoto wanaopata ruzuku ya utimizaji wa masharti ya elimu na ili ruzuku hiyo iendelee kutolewa kwa wanafunzi hao ni lazima mahudhurio yao yasiwe chini ya asilimia 80 kwa muhula, wasipohudhuria kuna adhabu inayotolewa ikiwa ni pamoja na kupunguzwa kwa ruzuku hiyo.

“ Miongoni mwa madhara ya watoto kutohudhuria masomo katika muhula husika kwa kaya zinazonufaika na TASAF kwa kupata ruzuku ya elimu ambayo inasaidia kaya hizo, ni kupungua kwa ruzuku na inapopungua uwezo wa kaya katika kujikimu na kufanya mabadiliko ya kiuchumi  unaathirika” amesema Sanga.

Kwa upande wake Bibi. Ngolo Buzenganwa mkazi wa kijiji cha Migato ambaye ni mnufaika wa Mpango wa TASAF III amewataka wazazi wenzake kufuatilia maendeleo ya watoto wao na kukagua daftari zao mara kwa mara ili ruzuku inayotolewa isipunguzwe na iwasaidie kuwawezesha kupata mahitaji muhimu ya shule kwa ajili ya watoto wao.

Katika hatua nyingine wanufaika wa Mpango wa TASAF III wameshukuru mpango huo kwa kutatua changamoto ya upungufu wa maji kwa kuwachimbia visima vya maji kupitia programu ya kazi za ajira za muda na kuomba kuongezewa idadi ya visima hivyo katika awamu nyingine ya utekelezaji wa mradi.

“Tunaishukuru sana TASAF kutuletea maji kwa visima hivi, tulikuwa tunatembea muda mrefu sana zaidi ya saa moja kufuata maji, lakini sasa hivi maji yapo karibu tena ni maji safi na salama” amesema Maila Limbu mkazi  wa Migato.

Naye Mhandisi wa Maji wa Halmashauri ya Wilaya ya Itilima,Goodluck Masige amesema Serikali Wilayani humo imeweka mpango wa kuviwekea pampu visima vyote 194 vilivyochimbwa kupitia mradi wa TASAF ili kuwarahisishia wananchi kupata maji kwa urahisi zaidi kuliko teknojia inayotuika sasa ya kuvuta kwa kamba.

Wilaya Itilima ni moja ya Wilaya tano zinazofanyiwa tathmini ya utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru kaya Maskini (TASAF III) katika awamu hii, tathmini inayofanywa na wataalam kutoka TASAF Makao Makuu, Benki ya Dunia na wadau wengine wa maendeleo (wadau washiriki wa mradi) ambao ni UNDP, UNFPA, ILO pamoja na Umoja wa Nchi za Ulaya(EU).

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa