• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wananchi Wahimizwa Kupenda Bidhaa Zinazozalishwa Nchini

Posted on: July 8th, 2017

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2017 Ndg. Amour Hamad Amour ametoa wito kwa wananchi kupenda na kuthamini bidhaa zinazozalishwa hapa nchini.

Amour ametoa wito huo wakati alipokuwa akitoa ujumbe wa Mbio za Mwenge wa Uhuru mara baada ya kuweka jiwe la Msingi Mradi wa kiwanda cha kuongeza thamani ya mazao Kilimo cha BUSEGA MAZAO LIMITED katika kijiji cha Mwanangi wilayani Busega.

Amesema wananchi watakapotumia bidhaa zinazozalishwa hapa nchini watasaidia kuongeza uzalishaji kutokana na kuwepo kwa soko la uhakika kwa viwanda na hatimaye kuongeza uchumi wa nchi.

Ameongeza kuwa wawekezaji wanapaswa kuzalisha bidhaa bora ambazo zitakidhi vigezo vya kiushindani sawa sawa na zile zinazotoka nje ya nchi ili kupunguza uingizwaji wa bidhaa za nje na kulifanya Taifa kuongeza pato lake.

“.....bidhaa ambazo zinazotoka nje zinapoingia hapa ndani zinakuwa na bei ndogo kuliko zinazozalishwa hapa nchini, ni  kwa sababu bado hatujajipanga kuzalisha kiushindani, sasa tuzalishe bidhaa zenye ushindani ili kuweza kuua soko la bidhaa ambazo zinatoka nje tuweze kukuza uchumi wa Taifa letu” alisema.

Aidha, amesema mwekezaji wa kiwanda cha BUSEGA MAZAO LIMITED atakapoanza uzalishaji  atoe kipaumbele cha ajira kwa wananchi wa wilaya ya Busega na ahakikishe wanafanya kazi katika hali ya usalama na kupewa haki na maslahi yao kama inavyostahili.

Kiongozi huyo wa Mwenge wa Uhuru 2017  pia amewataka wakazi wa Wilaya ya Busega na Mkoa wa Simiyu kwa ujumla kuhakikisha kuwa wanazalisha kwa wingi mazao yote yanayotakiwa katika kiwanda hicho ukiwepo mpunga na mahindi kwa kuwa kitatoa soko la uhakika na kupelekea ongezeko la pato la mtu mmoja mmoja.

Akisoma taarifa ya mradi wa kiwanda hicho,Ndg. Lazaro Japhet kutoka BUSAGA MAZAO LIMITED amesema Kiwanda hicho kitawasaidia wakulima kupata soko, kuhifadhi na kuongeza mazao yao.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe.Tano Mwera amesema Serikali wilayani humo iko tayari kushirikiana na wawekezaji ambao watakuwa tayari kuwekeza katika wilaya hiyo.

Sambamba na hayo Ndg.Amour Hamad Amour amewataka wananchi kufanya kazi kwa bidii, kulinda rasilimali za nchi na kuendelea kupambana na rushwa, dawa za kulevya, malaria na UKIMWI ili kuweza kufikia Tanzania ya Uchumi wa Kati.

Akizungumza na wananchi na wanafunzi katika  Shule ya Sekondari Mkula Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2017 amesisitiza wanafunzi wa shule za sekondari kuwa na Klabu za wapinga rushwa, mapambano dhidi ya dawa za kulevya, malaria na UKIMWI ili waweze kufikia malengo yao.

Mwenge wa Uhuru ukiwa Wilayani Busega umepitia jumla ya miradi 9 katika sekta ya Elimu, Afya, Maji,Utawala Bora, Viwanda na Maendeleo ya jamii, yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.5.

 


Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa