• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wananchi Simiyu Watakiwa Kushiriki Michezo Kuimarisha Afya

Posted on: November 28th, 2020

Mkuu wa Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu, Mhe. Benson Kilangi ametoa wito kwa wananchi na viongozi mkoani hapa kuona umuhimu wa kushiriki michezo kwa ajili ya kuimarisha afya.

Kilangi ameyasema hayo Novemba 28, 2020 katika Tamasha la Simiyu Jambo Festival lililofanyika katika Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, likihusisha mashindano ya baiskeli, mbio fupi , ngoma za asili na mashindano ya taaluma kwa wanafunzi wa shule za sekondari; alipokuwa akitoa salamu za Mkoa kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka.

"Hii michezo tunayoifanya pamoja na kwamba ni burudani tunapaswa kuelewa kwamba michezo ni afya; ni wajibu wetu kila mmoja kwa nafasi yake ahakikishe anashiriki michezo, siyo lazima iwe kama hii tu, hata nyumbani tunaweza kufanya mazoezi madogo madogo kama kukimbia, kuruka kamba na mengine kwa afya," alisema Kilangi.

Aidha, Kilangi aliongeza kuwa michezo ni ajira kwakuwa wapo watu wanajipatia vipato kupitia michezo na vile vile michezo ni biashara na inasaidia kujenga mahusiano na undugu katika jamii.

Akizungumzia Kauli Mbiu ya Tamasha la Simiyu Jambo Festival mwaka 2020 inayosema, “WAWEZESHE WANAWAKE NA WATOTO WA KIKE ILI KUWA NA DUNIA BORA” Kilangi amesema ni vema watoto wa kike na wanawake wakawezeshwa kwa kuwa ni wakombozi wa familia na ndiyo wanaorudisha maendeleo nyumbani kwa asilimia kubwa ikilinganishwa na wanaume.

Katika hatua nyingine Kilangi ametoa rai kwa wadau wakashirikiana na mkoa wa Simiyu kuona namna ya kuwa na matamasha yanayohusu michezo, sanaa na utamaduni kuanzia ngazi ya wilaya, ili kuendelea kuujenga Mkoa wa Simiyu katika nyanja mbalimbali.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Miriam Mmbaga amesema kwa sasa Tamasha hilo limekuwa likishirikisha washiriki kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini, huku akibainisha kuwa nia ya Mkoa ni kupata washiriki wa ndani na nje ya nchi ili litumike pia katika kutangaza na kukuza fursa mbalimbali za kiuchumi zilizopo Simiyu.

Naye Mwakilishi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu Duniani ( UNFPA) ambao ndiyo wadhamini wakuu, Dkt. Amir Batenga amesema Shirika hilo litaendelea kushirikiana na mkoa wa Simiyu katika masuala mbalimbali ya kuwawezesha watoto wa kike na wanawake katika nyanja mbalimbali kama kauli mbiu ya tamasha la Simiyu Jambo Festival mwaka 2020 inavyosema.

Kwa upande wake Mbunge wa Viti Maalum (Vijana), Mhe. Lucy Sabo ameupongeza uongozi wa Mkoa kwa maandalizi mazuri na kutoa rai kuwa Tamasha la Simiyu Jambo Festival liwe endelevu kwa ajili ya kuinua vipaji kwa vijana na kuwahamasisha kushiriki katika utamaduni, sanaa na michezo.

Baadhi ya washiriki wa Tamasha la Simiyu Jambo Festival ambalo linafanyika kwa mara ya tatu mkoani Simiyu, wamewashukuru waandaji kwa maandalizi mazuri na ambapo wamebainisha kuwa mwaka huu ulinzi umeimarishwa zaidi.

"Tunawapongeza waandaaji mwaka huu mashindano ni mazuri, Ulinzi umeimarika sana kuanzia tulipoanza, njiani kote mpaka tulipofika eneo la kumalizia, kwa hali ilivyokuwa hakuna ambaye angeweza kubebwa kwa namna yoyote ile ili kutafutiwa ushindi," alisema Paul Michael mshindi wa kwanza mbio za baiskeli wanaume kilomita 140.

Katika mashindano ya baiskeli washiriki kutoka mikoa ya Mwanza na Shinyanga wameonekana kung'ara zaidi ambapo Paul Michael kutoka Shinyanga ameibuka mshindi na kujinyakulia kitita cha shilingi 800,000/= na Laurencia Luzuba ameongoza upande wa wanawake na kujinyakulia shilingi 600,000/= , upande wa walemavu Emmanuel John kutoka Simiyu ameibuka kidedea na kujipatia kitita cha shilingi 200,000/=

MWISHO.

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/11/wananchi-simiyu-watakiwa-kushiriki.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa