• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wananchi Mwasubuya Simiyu Kubadili Maisha yao Kupitia Kilimo cha Umwagiliaji

Posted on: September 4th, 2018

Wananchi wa Kijiji cha Mwasubuya wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu wamesema Mradi wa Umwagiliaji wa Mwasubuya wenye ekari 514 utawasaidia kubadili maisha yao kiuchumi kwa kuwa wanatarajia kuongeza mavuno kutokana na kuanza kutumia zana za kilimo za kisasa katika uzalishaji kuanzia hatua ya kuandaa mashamba hadi kuvuna.

Wananchi hao wameyasema hayo baada ya makabidhiano ya zana za kilimo za kisasa zitakazotumika kuanzia hatua ya kuandaa mashamba mpaka kuvuna, kutoka Kampuni ya Agricom kwa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi ambayo imewadhamini wananchi walio katika mradi wa Umwagiliaji wa Mwasubuya, yaliyofanyika katika eneo la Mradi Kijiji cha Mwasubuya, Septemba 03, 2018.

Wamesema pamoja na kuongeza uzalishaji kutokana na uwepo wa maji ya uhakika ya Bwawa la Mwasubuya na matumizi ya zana bora, mradi huo ambao utajikita zaidi katika kilimo cha mpunga pia utawawezesha wananchi na hasa vijana kujiajiri kupitia kilimo cha mboga mboga, hatimaye kukuza kipato chao na Taifa kwa ujumla.

“Tumefurahi sana kupata mradi wa umwagiliaji, hii ni ajira kwetu hasa sisi vijana wenye nguvu, nina imani tukiutumia mradi huu vizuri utatubadilisha sisi kiuchumi kwa sababu mashine za kisasa tulizoletewa tutazitumia kulima eneo kubwa kwa muda mfupi, tutatongeza mavuno na kupata hela nyingi ” alisema Daniel Ntobi Mkulima wa Mwasubuya

“Nimeupokea mradi huu kwa furaha kabisa na nina uhakika kupitia mradi huu tutalima na kupata mazao mengi hatutakuwa na njaa lakini pia mazao mengine tutauza ili tujenge nyumba nzuri, tusomeshe watoto hata kijiji chetu kitabadilika, cha msingi hapa tuutumie vizuri” alisema Monica Severine Mkulima kutoka kijiji cha Mwasubuya

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Mhandisi. Wilbert Siogopi amesema zana za kilimo zilizokabidhiwa na Kampuni ya Agricom zitawasaidia wakulima kuongeza uzalishaji wa zao la mpunga na hivyo kuongeza pato la kaya zao na kukuza uchumi wa Halmashauri na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema dhamira ya Serikali ni kuufanya Mradi wa Umwagiliaji Mwasubuya kuwa wa mfano ambao watu kutoka sehemu mbalimbali za dunia watakuja kujifunza, ambapo amebainisha kuwa mpunga utakaolimwa utakuwa wa aina moja,utalimwa mara mbili kwa mwaka na hautatumia mbolea za viwandani.

Ameongeza kuwa pamoja na kilimo cha mpunga, Serikali mkoani humo imekusudia kufunga kinu cha kukoboa mpunga na kupanga madaraja ya mchele na kupitia mradi huo pia kutakuwa na ufugaji wa samaki katika Bwawa la Mwasubuya ambapo vifaranga vitawekwa na ufugaji kupitia vizimba utafanyika sambamba na kufuga samaki katika baadhi ya mashamba ya mpunga.

“Kwenye bwawa mle tutaweka vifaranga vya sangara, kambare na sato pia katika ekari zitakazolimwa ekari 10 zitatengwa ambazo mkulima atalima mpunga na kufuga samaki kwa wakati mmoja, wakati akivuna mpunga anavuna na samaki; tunataka kufunga kinu cha kukoboa mpunga na kupanga madaraja, nawaambia maisha yenu yatabadilika, hapa ni mahali tunataka kuiambia dunia Simiyu ni nini” alisema Mtaka.

Akizungumzia namna wakulima watakavyolipa deni la mkopo wa zana bora za kilimo kutoka Agricom, Mtaka amesema Halmashauri italima shamba lote ekari 514, itatoa mbegu kwa wakulima, itapanda na kuvuna na baadaye itachukua sehemu ya mavuno(gunia 10 kwa ekari) kutoka katika matarajio ya mavuno ya kati ya gunia 30 hadi 42 kwa ekari, ili kufidia gharama za uzalishaji na kurejesha deni.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Agricom, Bi Angelina Ngalula amesema kampuni hiyo inafanya kazi na Halmashauri na wakulima walio tayari na kubainisha kuwa imekopesha Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi mashine za kulimia, kupandia na kuvunia zenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 200 ambazo kwa mujibu wa makubaliano zitalipwa baada ya mavuno.

Mradi wa Umwagiliaji wa Mwasubuya una eneo lenye ukubwa wa ekari 700 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji na umesajiliwa kwa Jina la Umoja wa Umwagiliaji Mwasubuya (UMWASU) wenye wanachama 198.

MWISHO

 KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/09/wananchi-mwasubuya-simiyu-kubabili.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa