• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wakulima Mkoani Simiyu Wasisitizwa Kulima Mazao ya Biashara

Posted on: November 2nd, 2017

Mkuu wa mkoa wa Simiyu,Anthony Mtaka amewasisitiza wakulima Mkoani humo mazao ya biashara yenye tija hasa zao la pamba kwa kuzingatia Mkoa huo upo katika mchakato wa utekelezaji wa ujenzi wa kiwanda cha bidhaa za afya zitokanazo na zao la pamba.

Msisitizo huo ameutoa jana Wilayani Maswa katika ziara yake ya kuhamasisha kilimo kuelekea msimu wa kilimo mwaka 2017/2018 na kueleza kuwa wakulima wanapaswa kuutumia vema msimu huu kwa kulima zao la pamba ambalo litawapatia fedha nyingi.

Mtaka alieleza kuwa wakulima wa Maswa na Mkoa mzima wageuze ujenzi wa kiwanda cha bidhaa za afya kuwa ni fursa ya kujiongezea kipato kwa kuzalisha zaidi zao la pamba ambalo ndilo litakuwa malighafi kuu katika uzalishaji wa kiwanda hicho.

Aidha alisema katika msimu msimu huu mpya wa mwaka 2017/2018 wakulima hao wanatakiwa kuondoa mazalia ya pamba yaliyobaki mashambani mwao na kisha kulima kwa kufuata kanuni bora za kilimo hicho.

"Katika msimu huu ninawaomba wakulima wote waondoe mazalia ya zao la pamba yaliyobaki mashambani kwa kuyachoma moto ili wasije kuharibu na kuambukiza magonjwa katika mbegu mpya na bora watakazozitumia...pia katika kupanda mpande kwa kuzingatia sentimeta 90 hadi 40 zilizoainishwa kitaalamu kutoka mstari hadi mstari....alisema Mtaka

Aidha wakulima hao hawakusita kueleza kero zao na kuitupia lawama bodi ya pamba kwa kushindwa kusimamia zao hilo huku wakidai kutoichafua kwa kuweka maji na mchanga katika zao hilo.

Irene Joseph mkulima kutoka katika kata ya Kadoto alifafanua kuwa wakulima wamekuwa wakionewa na kusingiziwa visingizio vingi juu ya uchafuzi wa zao hilo ,huku akieleza tuhuma hizo kuwa si za kweli na kubainisha kuwa bodi ya pamba inapaswa kutimiza wajibu wake  katika kulisimamia zao la pamba na kutoa elimu ya kutosha kwa wakulima .

Nae afisa kilimo wa Wilaya ya Maswa Christopher Simwimba amewataka wakulima kutumia mbolea ya samadi katika kuongeza rutuba kwenye mashamba yao .

Afisa huyo aliongeza kusema kuwa wakulima wanatakiwa kubadilika na kulima kisasa ili waweze kuendana na falsafa ya serikali ya viwanda ambapo wakulima ndio wanategemewa wao kuwa ni wazalishaji wa malighafi za viwandani.

Nae mkuu wa Wilaya ya Maswa Dkt Seif Shekilage alisema kuwa katika kuhakikisha wanaboresha na kuliinua zao la pamba Halmashauri yake imeweza kuwasaidia vikundi vya vijana na wanawake wanajihusisha na kilimo kuwapatia mkopo wa Milioni 50 kwa vikundi 16 vinavyotarajia kulima zao la pamba kwa msimu huu.

Mkuu wa Wilaya ya Maswa Dk Seif Shekalage akitoa ufafanuzi wa namna Wilaya yake ilivyojipanga kuongeza uzalishaji wa zao la pamba.

Wakulima kutoka katika kata 36 za Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu wakiwa katika mkutano wa pamoja Viongozi wa Mkoa  na  Wilaya(hawapo pichani)  ukiwa na lengo la kujadili na kupokea maelekezo ya kilimo katika msimu mpya wa 2017/2018.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa