• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wananchi 1000 Wajitokeza Kuchimba Msingi wa Mabweni ya Shule ya Ufundi Simiyu

Posted on: May 11th, 2018

Wananchi takribani 1000 wa Kata ya Malambo wilayani Bariadi wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Mhe.Festo Kiswaga wamejitokeza  kuchimba msingi wa mabweni  ya Shule ya Sekondari ya Ufundi ya Mkoa wa Simiyu ambayo inayotarajiwa kuanza kujengwa mwezi huu .

Wakizungumza katika nyakati tofauti baadhi ya wananachi walioshiriki katika zoezi hilo wamempongeza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka kwa maono yake katika kuleta maendeleo ya elimu mkoani humo na kuahidi kuwa watahakikisha wanamuunga mkono ili malengo ya kuwa na shule ya vipaji maalum yanatimia.

“Tunamshukuru Mkuu wetu wa Mkoa kwa kuja na maono haya ya kuwa na shule ya Ufundi ya Mkoa na sisi kama wananchi wa eneo hili  tunamuunga mkono kiongozi wetu, nitoe wito kwa wananchi wenzangu kila mmoja aweze kuchangia alicho na uwezo nacho  ili tuweze kujenga shule yetu hii ikamilike na watoto wetu waanze kusoma” alisema Christina Matulanya Mkazi Malambo Bariadi.

Diwani wa Kata ya Malambo Mhe.Kitebo Kitebo amesema wananchi wa Kata ya Malambo kwa pamoja wameonesha ushirikiano toka walipotangaziwa kwa mara ya kwanza juu ya kuanza kwa ujenzi wa shule hiyo, hivyo akawaomba kuendelea kushirikiana mpaka shule hiyo ikamilike.

Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga amewashukuru wananchi wake na akawaomba waendelee kuonesha ushirikiano katika kufanikisha ujenzi wa shule hiyo ili wawe mfano bora kwa wilaya nyingine zitakapoanza kujenga shule za vipaji maalumu pia.

Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Bariadi Nicholaus Kasendamila amesema Jitihada hizo za Ujenzi wa Shule hiyo ya Mkoa zilizoanzishwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu lazima ziungwe Mkono ambapo amewataka Wananchi kuweka pembeni siasa kwenye suala hilo la Maendeleo

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka ambaye aliwatembelea Wananchi hao amesema Kuwepo kwa Shule hiyo ya Ufundi kutaleta chachu kubwa katika kuwapata watalaam wa fani mbalimbali katika utekelezaji wa azma ya Serikali ya awamu ya Tano ya Tanzania ya Viwanda na akawataka wazazi kuwasisitiza watoto wao kusoma kwa bidii.

“Mkoa wa Simiyu unajipambanua kama Mkoa wa viwanda ni lazima tuwe na shule ambazo watoto wetu kwenye mitaala yao wanapomaliza kidato cha nne wanakuwa na stadi za ufundi za kujiendeleza kimaisha, tunataka tujenge shule yenye karakana nzuri za ufundi watoto watakaopita hapa waweze kuendesha maisha yao, tunataka shule hii ijibu mahitaji ya mkoa” alisema

Aidha, Mtaka amesema hadi sasa wadau mbalimbali wamejitokeza kuchangia shule hiyo na mpaka sasa jumla ya shilingi milioni 157 zimetolewa na wadau hao ili kuunga mkono ujenzi wa shule hiyo na Serikali imetenga jumla shilingi milioni 58 kwa ajili ya ujenzi wa Jengo la Utawala.

Ameongeza kuwa baada ya kukamilisha shule hiyo ya Ufundi, Mkoa huo unatarajia kujenga shule ya Wasichana , Shule ya Wavulana na shule maalumu ya mchepuo wa Kilimo ambayo itatumika kama sehemu ya mazoezi kwa vitendo kwa Chuo cha Kilimo Sokoine(SUA).

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU TUKIO HILI FUNGUA KIUNGANISHI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/05/wananchi-wajitokeza-kuchimba-msingi-wa.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa