• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wanafunzi Simiyu Waomba Kambi za Kitaaluma Ziwe Endelevu

Posted on: April 14th, 2021

Wanafunzi wa shule ya sekondari Bariadi mkoani Simiyu wameomba viongozi wa mkoa na wadau wote wa elimu kuwa kambi za kitaaluma ziwe endelevu kwa kuwa zina matokeo chanya kwa katika ufaulu wa wanafunzi na ili mkoa uendelee kufanya vizuri katika mitihani yote ya Kitaifa.

Ombi hilo limetolewa tarehe 14 Aprili 2021 wakati wanafunzi hao walipopokea msaada wa chakula, shajala na taulo za kike kutoka Benki ya TPB vyote vikiwa na thamani ya shilingi 4,550,000/= ambavyo vimetolewa kwa jili ya wanafunzi wa kambi za kitaaluma kwa kidato cha sita mkoani hapa.

“Tunaomba kambi hizi ziwe endelevu maana zina mchango chanya kwenye ufaulu wa masomo yetu, miaka ya nyuma tulikuwa tukishika nafasi za mwisho kabisa lakini sasa hivi tumekuwa wa tatu Kitaifa; pia tuwaahidi tu kwamba kidato cha sita mwaka huu  hatutawaangusa tutashika nafasi ya kwanza,” alisema Godfrey Andrew mwanafunzi wa kidato cha sita.

“Tunashukuru kwa msaada huu wa vitu tulivyopewa lakini pia tunashukuru kwa jitihada za mkoa kuanzisha kambi ambazo zimetusaidia kuongeza ufaulu wetu, pamoja na ufaulu kambi hizi zimesaidia wanafunzi wengi kumaliza masomo yao pasipo kukatishwa na sababu za kijamii kwani muda mwingi wanakuwa shuleni,” Minza Kija mwanafunzi wa kidato cha nne

Awali akitoa taarifa ya elimu ya mkoa Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju amesema mkoa una mkakati wa taaluma wenye vipengele 12 na kimojawapo kikiwa kambi za kitaaluma ambazo zimechangia kuuweka mkoa katika mikoa kumi bora katika mitihani yote ya Kitaifa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mikopo wa Benki ya TPB, Bw. Henry Bwogi akikabidhi msaada wa chakula, shajala na taulo za kike kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TPB Benki amesema benki imetoa msaada huo kwa lengo la kuunga mkono juhudi za Serikali katika elimu.

Aidha, Bwogi ametoa rai kwa wanafunzi kujisomea kwa bidii ili waweze kufanya vizuri na kufikia ndoto zao ikiwa ni njia moja wapo ya kuthamini juhudi za viongozi wa Mkoa wa Simiyu na wadau mbalimbali katika elimu.

Akizungumza kwa niaba ya uongozi wa Mkoa, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Ekwabi Mujungu ameishukuru Benki ya TPB kutoa msaada huo ambao umeonesha ni namna gani wadau wa elimu wanatambua kazi inayofanywa na viongozi na wananchi wa mkoa wa Simiyu katika sekta ya elimu ambapo amewahakikishia kuwa msaada huo utatumika kwa malengo yaliyokusudiwa.

Vile vile Mujungu amewapongeza viongozi na watendaji wa idara ya elimu mkoa wa Simiyu kwa jitihada wanazofanya katika elimu ambazo zimechangia kuuweka mkoa wa Simiyu katika nafasi nzuri ya ufaulu kwa mitihani yote ya Kitaifa, huku akiwataka wanafunzi wasome kwa bidii ili waweze kufanya vizuri na kufikia lengo la mkoa la kushika nafasi ya kwanza katika mitihani yote.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2021/04/blog-post.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa