• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wanafunzi 7361 wa Kidato cha Nne Mkoani Simiyu Kuweka Kambi ya Kitaaluma mwezi Juni

Posted on: April 13th, 2018

Wanafunzi 7,361 wa kidato cha nne kutoka katika shule za sekondari Mkoani SIMIYU wanatarajia kuweka kambi maalum ya kitaaluma ili kujiandaa na Mtihani wa Taifa na kuweza kuinua kiwango cha ufaulu mkoani humo.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka wakati alipokuwa akifunga Kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi 1005 wa Kidato cha Sita kutoka shule 11 Mkoani humo, waliokuwa chini ya Wakuu wa Shule 11 na walimu mahiri 40, wilayani Maswa.

Lengo la kambi hii lilikuwa ni kutekeleza sehemu ya mkakati wa Mkoa huo wa kufuta daraja la nne na sifuri kwa kuwaandaa wanafunzi wa Kidato cha Sita Mkoani humo na Mtihani wa Taifa unaotarajiwa kufanyika mwanzoni mwa mwezi Mei.

Mtaka anasema baada ya kumalizika kambi hiyo ni matumaini ya Mkoa wa Simiyu kuona wanafunzi wanafaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza na kufuta sifuri huku akitangaza kuanza kwa kambi ya wanafunzi wa kidato cha nne.

“Tumemaliza kambi ya Kidato cha Sita, natangaza rasmi leo kuwa tutakuwa na  Kambi ya Kidato cha Nne na Darasa la Saba mwezi Juni Mwaka huu, wanafunzi 7361 wa kidato cha nne watakaa kwenye kambi siku 21, kila wilaya itakaa na wanafunzi wake na mimi kama Mkuu wa Mkoa nitayafungua makambi hayo” alisema

“Baada ya kambi hiyo tutachukua wanafunzi bora watano katika kila shule baada ya mtihani wa Mkoa kufanyika ambao watatengeneza kambi kiwilaya pia,  ili tuchakate na kupata wanafunzi bora watakaotengeneza daraja la kwanza kwenye mkoa” alisisitiza

Aidha, Mtaka amesema anashauriana na Maafisa Elimu kuona uwezekano wa  kutengeneza kambi kwa ajili ya wanafunzi 10 ambao wanafanya vibaya kwa kila shule ili waweze kusaidiwa  na baaaye Mkoa uweze kuondokana kabisa na sifuri.

Ameongeza kuwa pia mwezi Juni wanafunzi 36,156 wa darasa la saba wataweka kambi na kambi zote mbili zitafunguliwa kwa pamoja, hivyo akatoa taarifa kuwa wadau wote wa elimu na watu wenye mapenzi mema watakapoombwa kuchangia ili kuwezesha kambi hizo wakubali kuunga mkono suala hilo.

Afisa Elimu wa Mkoa wa SIMIYU, Julius Nestory ameahidi kuwa kufikia mwaka 2020 kutakuwa na Mapinduzi makubwa ya Sekta ya Elimu katika Mkoa huo.

Wanafunzi wa kidato cha sita waliomaliza kambi iliyochukua takribani siku kumi wamesema kukutanishwa pamoja kumewasaidia hasa kwenye mada na maswali yalikuwa yanawasumbua, hivyo kwa sasa wamejiandaa vizuri na watafanya  vizuri katika Mtihani wao wa mwisho.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa SIMIYU amesema Ofisi ya Mkuu wa Mkoa itatoa Shilingi Milioni Mbili kwa mwanafunzi atakayeingia katika kumi bora Kitaifa, Shilingi Milioni Tano kwa shule itakayokuwa miongoni mwa shule kumi bora na mwalimu mahiri atakayewezesha Alama A atapata Shilingi Laki mbili.

MWISHO

KUAPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA HAPA:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/04/wanafunzi-7361-kidato-cha-nne-simiyu.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa