• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Wakuu wa Shule Watakiwa kuwa Wabunifu Kuongeza Ufaulu

Posted on: August 5th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewataka Wakuu wa Shule mkoani humo kuongeza ubunifu ili kuongeza ufaulu wa wanafunzi katika shule zao.

Mtaka ameyasema hayo wakati alipokuwa akifunga mafunzo ya siku mbili kwa wakuu wa shule zote za Sekondari yaliyofanyika Mjini Bariadi katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Bariadi

 Amesema wakuu wa shule wanatakiwa kuwa wabunifu hususani katika mbinu mbalimbali zitakazosaidia kuwaandaa vizuri kitaaluma wanafunzi ikiwa ni pamoja na mazoezi na mitihani ya kujipima ya mara kwa mara, zitasaidia wanafunzi kufanya vizuri katika mitihani ya ndani na kitaifa.

“Kiongozi lazima uwe mbunifu, Mkiwa wabunifu kwenye shule watoto watafanya vizuri,mnapaswa kubuni mbinu na mikakati mbalimbali kwenye majaribio ya darasani, mitihani ya kujipima na  kubuni namna ya kuwapa motisha walimu wenu wapende kazi na kujiona ni wanafamilia katika shule mlizopo” amesema Mtaka.

Aidha, amewataka wakuu hao wa shule kujiwekea utaratibu wa kupita mara kwa mara madarasani kukagua kwa lengo la kujiridhisha, ikiwa walimu wanatimiza wajibu wao wa kuwafundisha wanafunzi kama inavyotakiwa badala ya kusubiri kuletewa taarifa.

Mkuu huyo wa Mkoa pia amewaasa wakuu hao wa shule kuwa na uongozi shirikishi ambao unajali pande zote kwa maana ya walimu, wanafunzi na wazazi ili waweze kujua kero na masuala mbalimbali yasiyowaridhisha na waweze kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa taratibu kuyapatia suluhu.

Vile vile Mtaka amesisitiza wakuu wa shule kufanya vikao na wazazi kwa kuwa wazazi wanayo nafasi kubwa ya kuchangia wanafunzi kufanya vizuri, hivyo akawataka wavitumie vikao kupata maoni ya wazazi katika masuala mbalimbali ya kuboresha maendeleo ya wanafunzi kitaaluma.

Sanjali na hilo amewataka Wakuu hao wa Shule kuzingatia sheria, kanuni , taratibu na kuchukua hatua stahiki pale inapobidi ikiwa ni pamoja na kutowaruhusu wanafunzi wajawazito au waliojifungua kuendelea na masomo.

Kwa upande wake Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl.Julius Nestory amesema katika mafunzo hayo ya siku mbili wakuu wa shule wameelimishwa juu ya sheria zote nne za Elimu, falsafa,nyaraka,kanuni mbalimbali za Elimu na sera mpya ya Elimu.

Nestory amebainisha pia kuwa wakuu  wa shule hao wamepewa mafunzo ya utunzaji wa nyaraka za Serikali, udhibiti wa vitendo vya rushwa, kusimamia shule na taaluma pamoja na utunzaji wa takwimu sahihi ambapo amewataka wakuu wa shule hao kutumia sheria zilizopo katika kusimamia shule kupitia mipango thabiti itakayotoa matokeo chanya.

Naye Magebu Bugacha Mkuu wa Shule ya Sekondari Mwantimba ameshukuru uongozi wa Mkoa kuona umuhimu wa kuwaandalia wakuu wa shule mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo ambayo yatawasaidia na kuwapa uzoefu katika kuendesha na kusimamia shule zao.

Akitoa shukrani kwa niaba ya Maafisa Elimu wa Wilaya za Mkoa huo, Afisa Elimu wa Wilaya ya Meatu, Mwl.Estomia Makyara amesema maelekezo yote ya Mkuu wa Mkoa aliyoyatoa wakati akifunga mafunzo hayo kwa Wakuu wa shule yatatekelezwa kwa uadilifu, ili mkoa wa Simiyu uwe ni miongoni mwa mikoa mitatu bora kwa ufaulu katika mitihani ya Kitaifa.

Jumla ya Wakuu wa shule 152 kutoka katika Halmashauri zote sita za Mkoa wa Simiyu wamepata  mafunzo hayo ambayo yalilenga kuwajengea uwezo katika usimamizi na uendeshaji wa shule za Sekondari.

Baadhi ya Wakuu wa Shule za Sekondari Mkoani Simiyu wakimsikiliza Mkuu wa mkoa huo, Mhe.Anthony Mtaka (hayupo pichani)alipozungumza nao wakati akifunga mafunzo ya siku mbili Mjini Bariadi.



Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa