• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Viongozi wa Umma Watakiwa Kuepuka Mgongano wa Kimaslahi Katika Maamuzi Wanayofanya

Posted on: December 4th, 2019

Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Jaji Mstaafu Harold Nsekela amewataka viongozi wa Umma kuangalia maslahi ya nchi katika maamuzi wanayofanya kwa kuwa kutanguliza maslahi binafsi kunasababisha mgongano wa kimaslahi unaopelekea kuiumiza nchi.

Jaji Nsekela ameyasema hayo wakati akizungumza na viongozi wa Umma katika mafunzo ya maadili na namna bora ya kujiepusha na mgongano wa maslahi  kwa Viongozi wa Umma mkoani Simiyu ambayo yamefanyika Desemba 04, 2019 Mjini Bariadi.

"Viongozi wa Umma wanapaswa kuzingatia kanuni na taratibu katiia maamuzi wanayofanya , ambazo zitasaidia kusiwepo mgongano wa kimaslahi ili kutenganisha matakwa binafsi na maslahi ya Umma katika kutekeleza majukumu, wakitanguliza maslahi binafsi wanaliumiza Taifa," alisema Jaji Nsekela.

Akizungumzia suala la ahadi ya uadilifu ambayo viongozi wa Umma hukiri mara baada ya kupewa nyadhifa mbalimbali na kuapishwa, Jaji Nsekeka amesema viongozi wa Umma wasikiri ahadi hiyo kama kasuku badala yake wawe waumini wazuri wa yale wanayoyakiri ikiwa ni pamoja na kufanya kazi zao kwa uadilifu.

Aidha, Jaji Nsekela amesema Viongozi wa Umma wanapaswa kuwa wakweli na wajaze kwa uhalali Tamko la Mali na Madeni huku akiwasisitiza kuondokana na dhana kwamba matakwa ya kisheria ya kujaza tamko hilo yanalenga kuwafilisi Mali zao kwa kuwa hakuna sheria inayozuia kiongozi wa Umma kuwa na Mali isipokuwa sheria inamtaka amiliki Mali halali zilizopatikana kwa njia halali.

Katika hatua nyingine Jaji Nsekela amewatahadharisha viongozi wa Umma kuachana na tabia ya kupokea zawadi kutoka kwa wanaowahudumia kwa kuwa jambo hilo ni kichocheo kikubwa cha rushwa, maana wao wanalipwa mishahara kwa kazi wanazofanya.

Awali akifungua mafunzo kwa Viongozi wa Umma mkoani Simiyu, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema mafunzo hayo yatawasaidia na kuwakumbusha viongozi hao kutoka huduma kwa wananchi kwa uadilifu pasipo upendeleo kwa kigezo cha dini, ukabila, kujuana na kutekeleza majukumu yao kwa wakati.

Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Lamadi wilaya ya Busega, Mhe. Laurent Bija amesema ili viongozi wa Umma waendelee kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu ni vema taasisi na mifumo dhabiti ya usimamizi ikaimarishwa na iwe endelevu.

Naye Katibu wa Idara ya Ukuzaji Maadili  kutoka Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma, Bw. Waziri Kipacha amesema ikitokea kiongozi wa Umma amekiuka masharti yaliyopo kwenye Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma, hatua ya kwanza ni Sekretarieti ya Maadili kufanya uchunguzi wa awali.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/12/viongozi-wa-umma-watakiwa-kuepuka.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa