• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Viongozi wa Riadha Kanda ya Ziwa Watakiwa Kuziandaa Timu Kikamilifu.

Posted on: January 20th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu ambaye pia ni rais wa chama cha riadha nchini Anthony Mtaka amewaagiza viongozi wa riadha kanda ya ziwa kuweka mpango mkakati endelevu wa kuwatambua na kuwaandaa kikamilifu wachezaji watakaoshiriki katika mashindano mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Mhe Mtaka ametoa kauli hiyo katika kikao na viongozi wa vyama vya riadha kanda ya ziwa kilichofanyika mjini Bariadi ambapo amesema chama cha riadha kinakabiliwa na mashindano mbalimbali ikiwemo mbio za nyika za dunia zitakazofanyika nchini Denmark, mashindano ya Afrika yatakayofanyika nchini Morocco pamoja na mashindano ya relay yatakayofanyika nchini Japan hivyo ni muhimu maadalizi yakafanyika mapema ili kuwaandaa wachezaji kisaikolojia na hatimaye waweze kurejea na ushindi.

Adha Mhe Mtaka amesema chama hicho kimeandaa utaratibu mzuri wa kuwapata wachezaji wenye viwango ambapo yatafanyika majaribio nchi nzima ili kuwawezesha viongozi na makocha kubaini vipaji vipya ili wachezaji hao waweze kujumuishwa kwenye timu ya Taifa.

“ Naomba niwahakikishia hatuwezi kupata wachezaji wazuri kama tutakaa tunalalamika, nendeni mkafanye majaribio katika ngazi za mikoa yenu, chagueni wachezaji wazuri ambao tutakuwa na uhakika watarejea na ushindi”.

“ Binafsi ninawaahidi nitawapa msaada wowote mnaohitaji, sote tunafahamu kanda ya ziwa kuna wachezaji wazuri sana, kinachohitajika ni kuweka mfumo mzuri wa kuwatambua na ndio maana tumeamua safari hii tutakuwa na makocha watano kwenye kambi zetu za taifa ambazo tunatarajia kuziweka katika mikoa ya Arusha na Pwani, mimi ninaamini tukidhamiria kuleta mabadiliko katika mchezo huu tunaweza ”, alisisitiza Mtaka.

Kwa upande wao wajumbe wa kikao hicho akiwemo mwanariadha  mkongwe ambaye ni mchezaji wa kwanza kushiriki katika michezo ya Olympic mwaka 1964, Mzee Thomas Daniel walimweleza rais wa chama hicho kuwa ukosefu wa viwanja vyenye ubora, kutokuwepo kozi ya makocha wa ngazi ya juu, uhaba wa vifaa pamoja na kozi maalumu kwa ajili ya makocha ni miongoni mwa changamoto zinazohitaji kupatiwa majawabu ili kuongeza hamasa katika mchezo huo.

Kikao hicho cha siku moja kilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa vyama vya riadha kanda ya ziwa kutoka mikoa ya Simiyu, Mwanza, Mara na Geita.


MWISHO

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa