• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

TRC Yaahidi Kuwarahisishia Wachambuzi wa Pamba Usafirishaji wa Marobota

Posted on: October 6th, 2019

Mkurugenzi wa shirika la reli nchini(TRC), Bw.Masanja Kadogosa amesema kuwa shirika hilo limejipanga kuhakikisha linarahisiha huduma za usafirishaji wa marobota ya pamba kwa njia ya reli lengo likiwa kuwapunguzia gharama wenye viwanda vya kuchambua pamba.

Kadogosa amesema hayo mara baada ya kutembelea viwanda vya kuchambua pamba vya Alliance kilichopo kata ya Kasoli na NGS katika wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu.

Pamoja na kupunguza gharama ameongeza kuwa njia hiyo ni salama na ya uhakika hata kipindi cha mvua mzigo unafika kwa urahisi bila matatizo ya aina yoyote huku akiongeza kuwa shirika la reli litaweka miundombinu itakayowarahisishia usafirishaji huo.

"Tumejipanga kuweka miundombinu itayowasaidia mizigo yakiwemo marobota ya pamba kusafirishwa kwa urahisi bila usumbufu wowote niwaombe wafanyabiashara watumie fursa hii ya reli kufanya shughuli mbalimbali zitakazowaingizia vipato hivyo kubadilisha maisha yao," alisema Kadogosa

Katika hatua nyingine aliongeza kuwa ni vyema jamii ione umuhimu wa kujenga viwanda vya nyama ili iwe iweze kusafirishwa nyama badala ya Mifugo ambapo mkoa wa Simiyu ni miongoni mwa mikoa yenye mifugo mingi nchini .

Awali akimkaribisha mkurugenzi huyo mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema kumekuwepo na changamoto kubwa inayowakabili wafanyabiashara hususan katika usafirishaji wa robota za pamba kwani wanalazimika kutumia magari jambo linalopelekea kusafirisha mizigo michache kwa gharama kubwa.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo amewasisitiza wafanyabiashara hao kuona haja ya kutumia reli kwani huduma hiyo imesogezwa karibu na itawasaidia kuepukana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya gharama za usafirishaji na potevu wa robota za pamba.

Aliongezea kuwa ni vyema ujenzi wa eneo la kuhifadhia marobota ya pamba eneo la Malampaka ukazingatiwa huku akiongeza kuwa ujio wa usafirishaji wa kupitia njia ya reli utawarahisishia na kuwapunguzia gharama wenye viwanda vya kuchambua pamba.

Ibrahimu Kadudu ni mrajisi mkoa wa Simiyu amesema kuwa makisio ya mkoa ilikuwa kuzalisha kilogramu milioni 180 na hadi kufikia septemba 22 2019, jumla ya pamba kilogramu milioni 148,836,601 zilikusanywa kwenye vyama vya ushirika ,pamba iliyosafirishwa ni kilogramu milioni 116,391,208, iliyolipiwa kati ya pamba iliyosafirishwa ni kilogramu milioni 85,166,453 , kilogramu milioni 31,106,816 zilisafirishwa bila kulipiwa huku kiasi kilogramu milioni 32,445,393 zikiwa bado kwenye maghala na kwa baadhi ya wakulima.

Kwa upande wake meneja wa kiwanda cha kuchambua pamba cha Alliance ambaye pia ni katibu wa wanunuzi nchini Boaz Ogolla alisema kuwa uzalishaji umeongezeka ambapo umesababisha uhitaji mkubwa wa magari ya kusafirishia marobota ya pamba huku akitolea mfano kiwanda cha ni Alliance.

“ Kiwanda hiki kinazalisha robota 400 kwa siku na zinazosafirishwa kwa siku ni robota 200 hivyo ujio wa usafirishaji kwa njia ya reli utamaliza changamoto hiyo maana behewa moja lina uwezo wa kubeba maroboto 90 tofauti na gari lina uwezo wa kubeba marobota 25,” alisema Ogola.

Sambamba na hayo ameongeza kuwa usafirishaji huo utawapunguzia gharama ambazo sio za lazima na kuwa awali changamoto ya usafirishaji iliwalazimu kulipia mizigo kwa gharama kubwa ambapo kupitia reli watasafirisha kwa gharama nafuu hivyo kutawawezesha na wao kupata faida kwenye biashara zao.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/10/trc-yaahidi-kuwarahisishia-wachambuzi.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa