• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Tizeba aitaka SIDO kuwapatia wakulima zana bora kuongeza thamani ya bidhaa zao

Posted on: October 25th, 2018

Waziri wa Kilimo Mhe. Dkt Charles Tizeba ameliagiza shirika la viwanda vidogo nchini SIDO kuhakikisha inawawekea wakulima mazingira bora ya utekelezaji wa shughuli za kilimo ikiwemo kupanua wigo wa upatikanaji wa zana bora zitakazoongeza thamani ya mazao yao na hivyo kuwajengea uwezo wa kupata soko la uhakika ndani na nje ya nchi.

Waziri Tizeba ametoa agizo hilo katika ziara yake ya kukagua mabanda ya maonesho ya SIDO kitaifa yanayofanyika katika viwanja vya Nyakabindi mkoani Simiyu na kusema kuwa kwa muda mrefu wakulima wamekuwa wakitumia teknolojia zilizopitwa na wakati zikiwemo za kusindika mazao ya kilimo pamoja na kukoboa mpunga jambo ambalo limekuwa likipunguza ubora wa bidhaa hizo.

Aidha waziri Tizeba amesisitiza kuwa njia pekee itakayosaidia kumkwamua mkulima ni kuhakikisha anajengewa uwezo na pia anawezeshwa kupata vifaa vya kisasa kwa bei nafuu hatua ambayo amesema utekelezaji wake unategemea ushirikiano na taasisi mbalimbali zikiwemo za fedha, kilimo na viwanda.

“ Ninahitaji kuona taasisi zote zinazoguswa na shughuli za kilimo zinaweka mikakati ya kumsaidia mkulima, kwa upande wenu SIDO hakikisheni wakulima hawa wanapata mashine za kisasa za kukoboa mpunga na kusindika vyakula na pia Wizara ya Viwanda biashara na uwekezaji iwasaidie masoko pia taasisi za fedha ziwasaidie kupata mikopo, alisisitiza Waziri Tizeba’’.

Kwa upande wake mkuu wa mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka amewashauri wajasiliamali wanaoshiriki katika maonesho hayo kubadilishana ujuzi ili kila mmoja aweze kupata mbinu stahiki za kuboresha biashara yake.

Mheshimiwa Mtaka amesema kuwa wiki moja ya maonesho hayo ni sawa na darasa kwa wajasiliamali ambapo wataweza kukutana na wenzao halikadhalika wapata ushauri kutoka kwa wataalamu mbalimbali kuhusu namna ya kuboresha shughuli zao huku akiwasisitiza wananchi waendelee kujitokeza kushuhudia maonesho hayo zikiwa zimebaki siku tatu kabla hayajahitimishwa.

Maonesho ya Viwanda Vidogo  SIDO KItaifa yenye Kauli Mbiu: “Pamoja Tujenge Viwanda Kufikia Uchumi wa Kati”  yanatarajiwa kufikia kilele chake tarehe 28 Oktoba , 2018.

MWISHO

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa