• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu Yazindua Upimaji wa Maeneo ya Wakulima, Wafugaji kwa Kutumia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)

Posted on: September 20th, 2018

Mkoa wa Simiyu umezindua Mpango wa kupima maeneo ya wafugaji na wakulima kwa kutumia teknolojia ya kisasa ya ndege nyuki (drones) lengo likiwa ni kuwawezesha kuyatambua maeneo yao na kupewa hati miliki na baadaye kuyawekea miundombinu muhimu ya ufugaji na kilimo na kuondokana na migogoro kati ya wakulima na wafugaji.

Zoezi hilo limezinduliwa na  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Anthony Mtaka katika kata ya Ng’hoboko wilayani Meatu na linatekelezwa Chini ya Serikali kwa Kushirikiana na Taasisi Ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii (ESRF).

Amesema Mkoa huo ndiyo unaoongoza kwa kilimocha pamba nchini na ni miongoni mwa mikoa yenye ng’ombe wengi nchini, kwa kuwa wakulima na wafugaji wanamiliki ardhi ni vema maeneo yao yakapimwa wakapewa hati miliki na baadaye watalaam wa ardhi wawasaidie kuandaa mpango wa matumizi bora ya ardhi.

Ameongeza kuwa wafugaji wa mkoa wa Simiyu wamekuwa wakitozwa faini katika maeneo mbalimbali hivyo ili kuondokana na kadhia hiyo maeneo yao yakipimwa na wakaweka miundombinu muhimu kama vile mabwawa, visima, majosho na maeneo ya malisho wataondokana na uchungaji wa mifugo na kwenda kwenye ufugaji wenye tija

“Tungehitaji mpime mashamba yenu yakishapimwa mtapewa hati, watalaam wa halmashauri watawatengenezea mpango wa matumizi bora ya ardhi na kuwashauri namna sahihi ya uwekeaji wa miundombinu kama majosho, mabwawa, visima ili muwe wafugaji wenye tija ambao hamtapigwa faini wala kuibiwa ng’ombe” alisema.

Kwa upande wake Mkuu wa Mfumo kutoka Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) Bw. John Kajiba amesema upimaji kwa kutumia teknolojia ya ndege nyuki utafanyika  kwa urahisi  na haraka zaidi na ikilinganishwa na upimaji wa watu moja kwa kwa moja.

“Uzuri wa kutumia ndege nyuki ni kwamba tutatumia muda mfupi sana kupima eneo kubwa kwa wakati mmoja mfano,  eneo ambalo lngeweza kupimwa na watu wane kwa muda wa siku nne drone(ndege nyuki) inafanya kwa muda wa siku moja” alisema.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Meatu, Mhe. Pius Machungwa amesema upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji utawasaidia kutatua migogoro kati ya wakulima na wafugaji na kupata hati ziatazowasaidia kuchukua mikopo kwenye taasisi za kifedha na kufanya shughuli za maendeleo kupitia maeneo yao

Nao wananchi wa Meatu wanasema wameupokea mpango huo kwa mikono miwili  kwa sababu watakuwa na uhakika wa umiliki wa maeneo yao baaada ya kupewa hati ambazo pia wamesema zitawasaidia kukopa mitaji ya kufuga na kulima kisasa na kwa tija.

“ Tumeupokea mradi huu kwa mikono miwili maana tutakapopimiwa maeneo yetu tutakuwa tunakopesheka kwenye taasisi za fedha, vile vile tutakuwa tumeondokana na migogoro kati ya wakulima na wafugaji kwa sababu maeneo yetu yatakuwa na mipaka iliyo wazi na kila mmoja atakuwa na hati ya kumili eneo lake” alisema John Mchagula mfugaji kutoka Kijiji cha Ng’hoboko

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSUS HABARI HII FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/09/simiyu-yazindua-upimaji-wa-maeneo-ya.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa