• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu yakabidhiwa Zahanati na Shirika la Life Ministry

Posted on: June 4th, 2018

Shirika la Kikristo la Life Ministry limekabidhi Zahanati kwa Uongozi wa Mkoa wa Simiyu ambayo imejengwa katika Kijiji cha Itubukilo wilayani Bariadi.

Akisoma taarifa ya makabidhiano ya zahanati hiyo mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka, Mkurugenzi wa Life Ministry Tanzania, Bw. Dismas Shekalaghe amesema shirika hilo lilipokea zahanati hiyo kutoka kwa wananchi ambao walianza kujenga kwa nguvu zao na kuifikisha hatua ya renta, hadi kufikia hatua za ukamilishaji wa zahanati hiyo Shirika la Life Ministry limetoa kiasi cha Shilingi milioni 71.

Amesema pamoja na zahanati hiyo, shirika hilo limefanya mengi mkoani Simiyu ikiwa ni apamoja na kutoa vifaa tiba Hospitali Teule ya Mkoa vyenye thamani ya shilingi milioni 40, huduma za macho na kutoa miwani bure, kutoa baiskeli zaidi ya 20 kwa walemavu, kugawa vifaa mbalimbali kwa makundi mbalimbali wakiwemo watoto wenye ualbino, kuwezesha vikundi vya bustani zaidi ya 40 katika kilimo cha umwagiliaji kwa njia ya matone na kuchimba visima virefu 12 vyenye thamani ya shilingi milioni 300.

Akizungumza mara baada ya makabidhiano hayo, Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ameishukuru Life Ministry kwa msaada wa zahanati hiyo na kuwahakikishia kuwa mara tu itakapokamilika Serikali itahakikisha Zahanati hiyo inafanya kazi na itapeleka watoa huduma za afya ili wananchi waanze kupata huduma.

"Niwakikishie tu kuwa Serikali itahakikisha Zahanati hii inafanya kazi kwa kuleta wataalam na bahati nzuri Serikali imekubali kuajiri watu wa Sekta ya Afya" alisema Mtaka.

Mtaka amesema Taasisi za Dini zimekuwa zikiunga mkono kazi mbalimbali zinazofanywa na Serikali katika kuwaletea wananchi maendeleo na akaiomba Life Ministry kuendelea kusaidia katika ujenzi wa Vituo vya kutolea huduma za Afya, ili kusaidia uboreshaji wa huduma za Afya mkoani Simiyu, kwa kuwa mkoa huo una uhitaji mkubwa wa vituo vya afya.

" Mkoa wetu tuna asilimia chini ya 40 ya vituo vya Afya, Kama ni jambo ambalo litakuwa ndani ya uwezo wa Taasisi ningeomba muendelee kutusaidia kwenye sekta ya Afya; zipo juhudi za Serikali katika uimarishaji wa sekta ya Afya hususani kwenye ujenzi wa Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali lakini washirika kama Taasisi za Dini bado tunawahitaji kwa kuwa mmekuwa mkono wa pili kwenye kuunga mkono juhudi za Serikali" alisisitiza.

Akizungumza kwa niaba ya Wananchi wa Itubukilo, Diwani wa Kata ya Itubukilo Mhe. Mayanda Makenzi akiishuku Life Ministry kwa kukamilisha ujenzi wa zahanati hiyo ambayo amesema itawaondolea adha wananchi wake kutembea mwendo mrefu kufuata huduma za Afya.

Naye Diwani wa Viti Maalum Mhe. Juliana Lucas amesema ukamilishaji wa zahanati hiyo utawasaidia sana wananchi kupata huduma karibu hususani wanawake ambao watapata huduma za afya ya uzazi na kupata msaada wa karibu wakati wa kujifungua na hivyo kupunguza vifo vya wakina mama na watoto.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Bw. Abdallah Malela amesema Zahanati hiyo ya Itubukilo itafunguliwa rasmi na kuanza kutoa huduma Julai Mosi, 2018.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA KIUNGANISHI:- https://simiyuregion.blogspot.com/2018/06/simiyu-yakabidhiwa-zahanati-na-shirika.html


Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa