• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu Yafunga Kambi ya Kitaaluma Kuchukua Tahadhari Dhidi ya Corona

Posted on: March 17th, 2020

Uongozi wa Mkoa wa Simiyu umefunga kambi ya Kitaaluma kwa wanafunzi wa kidato cha Sita mwaka 2020 iliyokuwa ikifanyika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Maswa , ikiwa ni sehemu ya tahadhari dhidi ya Homa kali ya Mapafu inayosababishwa na Virusi vya Corona.

Akifunga kambi hiyo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini amesema uongozi wa mkoa umefikia hatua hiyo kuchukua tahadhari kama ilivyoelekezwa na viongozi mbalimbali wa Kitaifa juu ya kuzuia mikusanyiko ya watu wengi isiyo ya lazima katika kipindi hiki ambacho kumeripotiwa idadi ya watu kadhaa kubainika kuwa na virusi vya Corona katika nchi mbalimbali.

“Kutokana na Maelekezo ya Serikali Mkoa umeona kambi hii ifungwe kwa ajili ya tahadhari dhidi ya Corona,  Mhe. Rais amesitisha mbio za Mwenge wa Uhuru kwa mwaka 2020, Mhe. Waziri Jafo amesitisha UMISETA na UMITASHUMTA na tahadhari mbalimbali zimeendelea kutolewa na Serikali ikiwemo ya kuzuia mikusanyiko; sisi hapa tuna wanafunzi  takribani 1000 kutoka shule 10 hivyo tumekubaliana kwa pamoja tuifunge kambi hii,” alisema Sagini.

Aidha, Sagini amesema pamoja na kambi za kitaaluma kufungwa Mkoa utaendelea kusimamia utekelezaji wa mkakati wa taaluma wa mkoa ili walimu, wanafunzi na wadau wengine wa elimu waweze kutimiza wajibu wao kuhakikisha Mkoa unatimiza adhma yake ya kuwa miongoni mwa mikoa itakayofanya vizuri katika mitihani yote ya Kitaifa.

Kwa upande wake Afisa Elimu wa Mkoa wa Simiyu, Mwl. Ernest Hinju amesema wanafunzi hao walitakiwa kukaa kambini muda wa wiki sita kwa ajili ya maandalizi ya Mtihani wa Taifa unaotarajiwa kufanyika mwezi Mei 2020, hivyo pamoja na kusitisha kambi hiyo walimu wamehimizwa kutimiza wajibu wao katika ufundishaji na wanafunzi wametakiwa kwenda kusoma kwa bidii ili kufikia lengo la Mkoa.

Awali akitoa elimu ya ugonjwa wa homa ya mapafu unaosababishwa na virusi vya Corona kwa wanafunzi na walimu kabla ya kambi kufungwa, Afisa Afya wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Reuben Malimi amesema ugonjwa huo hauna tiba matibabu yanayofanyika yanazingatia dalili zinazoonekana kwa mgonjwa, hivyo ni vema kila mmoja  akachukua tahadhari kwa kuzingatia maelekezo na elimu inayotolewa na wataalamu wa afya katika maeneo mbalimbali.

Nao wanafunzi wa Kidato cha Sita wa Mkoa wa Simiyu wameshukuru uongozi wa Mkoa kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona kwa kutoa elimu kuhusu Corona  kabla ya kufunga kambi, huku wakieleza namna ambavyo kufungwa kwa kambi kunaweza kuathiri malengo yao waliyojiwekea.

“Tunashukuru uongozi wa Mkoa kutoa elimu  na kuchukua tahadhari ya Corona kwa kufunga kambi ni hatua ya kutuhakikishia usalama, lakini kambi ilitusaidia kujua namna ya kujibu maswali ya mtihani wa Taifa na kujifunza mada ngumu tulizoshindwa shuleni kupitia kwa walimu mahiri, tutatumia muda huu kujisomea kwa bidii ili tufaulu vizuri mtihani wa Taifa,” alisema Isack Ndassa kutoka Shule ya Sekondari Kanadi Itilima.

MWISHO

 KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/03/simiyu-yafunga-kambi-ya-kitaaluma.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa