• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Simiyu Yadhamiria Kuwakomboa Wafugaji kwa Kuwasaidia wafuge Kisasa

Posted on: September 28th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.  Anthony Mtaka amewataka wataalamu wa mifugo na kilimo kuachana na utamaduni wa kufanya kazi kwa mazoea huku akiwataka kuongeza ubunifu sambamba na kupanua wigo wa kutoa elimu kwa wafugaji ili kuongeza ufanisi katika sekta hiyo ambayo ni ya pili katika kuchangia pato la mkoa.

Mtaka ametoa kauli hiyo wakati akifungua warsha ya kujadili maendeleo ya sekta ya mifugo na mnyororo wake wa thamani iliyofanyika mjini Bariadi na kusema kuwa baada ya warsha hiyo anategemea kuwaona maafisa ugani na wataalamu wa mifugo wakiwaelimisha zaidi wafugaji mbinu bora za ufugaji wa kisasa ambazo zitabadili sura ya mkoa huo.

“ Hivi kwa nini tunakuwa watu wa kusifia nchi nyingine badala ya kujipanga ili na sisi hatimaye tuweze kuwa kama wao, utasikia mtu anasema ukitaka kujifunza mbinu bora za ufugaji nenda Ethiopia au Botswana, hivi sisi tunashindwa nini kuwa kama wao”, alihoji Mtaka.

Akisisitiza umuhimu wa kuwekeza katika elimu kwa wafugaji Mtaka  amewasisitiza wataalamu wa mifugo katika halmashauri  zote za wilaya mkoani Simiyu kuhakikisha wanatumia ubunifu wao kadiri iwezekanavyo kuwajengea uwezo wafugaji ili waweze kunufaika na sekta hiyo halikadhalika waweze kuchangia katika ukuaji wa sekta ya viwanda vitakavyohitaji malighafi zinazotokana na mifugo.

Kwa upande wake mwakilishi wa balozi wa Ireland ambaye ni mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Ubalozi huo Dkt. Niall Moris amesema nchi yake itaendelea kushirikiana na Tanzania katika suala zima la kuwajengea uwezo wataalamu wa mifugo mkoani Simiyu ili na wao wawe chachu ya kuisambaza elimu na ujuzi huo kwa wafugaji.

Dkt. Niall ameongeza kuwa serikali ya Ireland imevutiwa kushirikiana na mkoa wa Simiyu kutokana na mipango yake mizuri na sera zenye mwelekeo unaotia matumaini ya kumkomboa mfugaji na kuongeza kuwa hiyo ndio njia pekee itakayosaidia kuleta mapinduzi katika sekta ya mifugo.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa tume ya Sayansi na teknolojia Dkt. George Mulamula amesema mabadiliko katika sekta ya mifugo yatasaidia kuleta msukumo katika sekta ya viwanda mkoani Simiyu na kusisitiza kuwa ongezeko la malighafi zitokanazo na mifugo zitaongeza msukumo kwa serikali na wadau wa maendeleo kufungua viwanda vingi zaidi.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa