• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Shirika la Maendeleo la Uingereza Latoa Shilingi Bilioni 1.7 kwa Ajili ya Ujenzi wa Miundombinu ya Elimu Simiyu

Posted on: February 22nd, 2018


Shirika la Mendeleo la Uingereza (DFID) kupitia Mpango wa Kuboresha Elimu Tanzania(EQUIP-T) limetoa jumla ya shilingi bilioni 1.7  kwa ajili ya ujenzi wa Miundombinu ya Elimu katika Halmashauri zote za mkoa wa Simiyu.

Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka wakati wa hafla fupi ya makabidhiano na vyerehani 50 kutoka Ubalozi wa China, kusaini hati ya makubaliano ya ujenzi wa Bweni la Wasichana Shule ya Sekondari Nkoma Itilima, Makabidhiano ya. Hundi ya Shilingi Milioni 178 kwa ajili ya ujenzi wa bweni hilo zilizotolewa na Balozi wa China, na uwasilishwaji wa Taarifa za mashirika wadau wa Maendeleo mkoani Simiyu(DFID, AMREF na UNFPA), ambayo ilishuhudiwa na Makamu wa Rais wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan.

Mtaka amesema fedha hizo zimeshapokelewa katika Akaunti za Halmashauri zote za Mkoa huo na wiki ya kuanzia tarehe 26/02/2018 Halmashauri hizo zinaanza kujenga miundombinu ya Elimu.

Mtaka ametoa shukrani zake kwa Shirika hilo ambalo amesema limechangia kwa kiasi kikubwa mabadiliko katika Elimu na kuufanya mkoa wa Simiyu kutoka kwenye nafasi za mwisho kwenye ufaulu mpaka kufikia nafasi ya 11 kwa mwaka 2017.

“ Tunawashukuru sana DFID kwa namna wanavyotusaidia katika Sekta ya Elimu kwenye mkoa wetu,  DFID kupitia EQUIP wametoa IPAD(Vishikwambi) kwa kila Mkuu wa Shule ndani ya mkoa Simiyu, Kila Mratibu wa Elimu wa Elimu Kata amepewa  pikipiki na anapewa posho ya shilingi 206,000/=  kila mwezi kwa ajili ya kununua mafuta ya kuwawezesha  kutembelea  shule zao,  sisi kama mkoa tunawashukuru sana” alisema Mtaka.

Akitoa taarifa ya utendaji kazi wa Shirika la Maendeleo la Uingereza (DFID) Bi. Elizabeth Arthy amesema Shirika hilo litaendelea kuunga mkono juhudi za Serikali  na kuhakikisha wanashiriki katika kuinua ubora wa elimu kwa watoto wa Mkoa wa Simiyu.

Naye Balozi wa China hapa nchini Mhe. Wang Ke aliyekabidhi vyerehani 50 kwa ajili ya Kikundi cha Wanawake Mjini Bariadi  amempongeza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka kwa jinsi anavyojishughulisha katika kuwaletea wananchi wa Mkoa wa Simiyu maendeleo na akaahidi kuendelea kushirikiana na mkoa huo katika nyanja mbalimbali.

Kwa upande wake Mwakilishi Mkazi wa Shirika lilaloshughulikia Idadi ya Watu Duniani(UNFPA), Bi. Jacqueline Mahon amewapongeza viongozi wa mkoa wa Simiyu wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo, Mhe.Anthony Mtaka na akaahidi kuendelea kuunga mkono juhudi za maendeleo mkoani humo kupitia huduma za afya ya uzazi kwa wananwake na vijana.

Akitoa shukrani kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Simiyu,  Mbunge wa Jimbo la Bariadi Mhe.Andrew Chenge, aliyashukuru mashirika hayo na Balozi wa China ambao ni wadau wakubwa wa maendeleo mkoani humo katika Sekta ya elimu, afya na viwanda na kubainisha kuwa mkoa huo una kiu ya maendeleo ni hivyo umejipanga kwenda kwa kukimbia wakati wengine wanatembea.

MWISHO

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa