• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Shilingi Bilioni 2.3 Zatolewa Kwa Walengwa wa TASAF 28984 Simiyu

Posted on: September 24th, 2020

Serikali imetoa jumla ya shilingi 2,327,259,225 kwa walengwa  wa TASAF III awamu ya pili wapatao  28984 kupitia mpango wa kunusuru kaya maskini katika kipindi cha mwezi Julai hadi Oktoba mwaka 2020 katika vijiji 376 mkoani Simiyu.

Hayo yamebainishwa na Mratibu wa TASAF mkoa wa Simiyu, Bw. Nyasilu Ndulu  Septemba 23, 2020 wakati wa zoezi la uhawilishaji fedha kwa walengwa wa TASAF wa kijiji cha Mwamishali wilayani Meatu.

“Fedha za walengwa tulizopokea ni shilingi 2,327,259,225 na hizi ni fedha za awamu mbili, mwezi Julai-Agosti na Septemba-Oktoba na zinalipwa kwa awamu moja;  fedha hizi zimefika kipindi muafaka cha maandalizi ya msimu wa kilimo nawashauri wazitumie vema katika maandalizi ya shughuli za kilimo lakini wajiwekee utaratibu wa kuwekeza kwenye shughuli za uzalishaji,” alisema Nyasilu.

Akizungumza na walengwa wa TASAF katika Kijiji cha Mwamishali  Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga ametoa rai kwa walengwa wao kuwa na nidhamu ya matumizi ya fedha hiyo ya ruzuku wanayopata ili waweze kufikia malengo yao.

“Ninawasihi muendelee kujiamini na kila mmoja atambue kuwa anaweza, uwezeshaji ndiyo huu umeletwa na serikali hivyo ni kila mmoja akijiamini kuwa atafanikiwa kupitia kazi anayofanya atafanikiwa, kama mtu anafuga kuku, mbuzi, au ng’ombe akiwatunza vizuri akisaidiwa na wataalam wa halmashauri mtakuza vipato vyenu na mtafikia malengo yenu,” alisema Mmbaga.

Afisa Kilimo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Kija Kayenze amesema ruzuku ya  fedha zilitolewa kwa walengwa wa TASAF zimefika katika kipindi muafaka, ambapo msimu wa kilimo unatarajiwa kufunguliwa Oktoba Mosi; huku akitoa wito kwa walengwa kutumia fedha hizo katika uandaaji wa mashamba, ununuzi wa mbegu bora ili waweze kupata mavuno bora.

Nao baadhi ya walengwa wa TASAF wameishukuru Serikali kwa kutoa ruzuku ya fedha ambazo zimewasaidia kuanzisha miradi midogo midogo hususani katika kilimo, ufugaji na ujasirimali ambayo inawawezesha kupata mahitaji yao ya kila siku na kuweka akiba kwa ajili ya baadaye.

“Naishukuru serikali kutusaidia kupitia TASAF, nilikuwa nafanya vibarua kupata hela ya matumizi na kuwanunulia wanangu mahitaji ya shule, lakini nilipoanza kupata hela za TASAF nikawa nazitunza baadaye nikanunua ng’ombe wawili ambao sasa hivi wamezaa, nategemea kuwauza wawili ili ninunue bati za kuezeka nyumba yangu na kupata mtaji,” alisema Sikitu Zengo mkazi wa Kijiji cha Mwamishali wilayani Meatu.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/09/zaidi-ya-shilingi-bilioni-23-zatolewa.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa