• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Serikali yawahakikishia Wafanyabiashara Simiyu Upatikanaji wa Maji, Umeme

Posted on: December 31st, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewahakikishia wafanyabiashara mkoani hapa kuwa Serikali itatatua changamoto ya upatikanaji wa huduma ya maji na umeme kupitia mradi wa maji wa ziwa Victoria, uimarishwaji wa mamlaka za maji na kujengwa kwa vituo vya kupozea umeme.

Mtaka ameyasema hayo wakati ufunguzi wa hoteli ya Sweet Dreams iliyoko Mjini Bariadi na kumpongeza mfanyabiashara John Sabu kwa uwekezaji huo.

Amesema Mkoa unaendelea kuimarisha vyanzo vya maji na mamlaka za maji na kufikia mwaka 2020 maji kutoka Ziwa Victoria yatakuwa yameshafika katika makao makuu ya mkoa, huku akibainisha kuwa tatizo la umeme litatatuliwa na ujenzi wa vituo vya kupozea umeme.

“Sisi tuna mradi mkubwa wa maji wa  Ziwa Victoria ambao (kwa maelezo ya Waziri wa Maji) mpaka mwezi Februari 2019 watakuwa wametangaza zabuni ya ujenzi wa mradi huo ili maji yafike hapa, kwa kuanza mpaka kufikia mwaka 2020 maji yatakuwa yamefika makao makuu ya mkoa”

“Kwenye umeme tumezungumza na watu wa Wizara ya Nishati, tutajengewa (sub-stations) vituo viwili vya kupozea umeme, kwa kuanzia kimoja kitajengwa mwaka huu kwa hiyo tutakuwa na umeme wa uhakika” alisisitiza Mtaka.

Katika hatua nyingine Mtaka amewataka Wakuu wa Wilaya kuwalinda wafanyabiashara wakubwa na wadogo na kuwasaidia kutafsiri sheria, miongozo na taratibu zinazopaswa kuwasaidia kufanya biashara zao katika mazingira mazuri, huku akisisitiza biashara ziendelee kufanyika saa 24.

Kwa upande wao Wafanyabiashara wamempongeza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa kuwaruhusu kufanya biashara saa 24 na wakamuahidi kuwa wataendelea kuwekeza katika ujenzi wa vitega uchumi mbalimbali ikiwemo hoteli za kisasa na kuendelea kuwa walipa kodi waaminifu.

“Tunamshukuru Mhe. Mkuu wa mkoa kwa kuruhusu wafanyabishara tufanye biashara zetu saa 24 tunamuahidi kuwa tutaendelea kufungua biashara mbalimbali kama hoteli  ili kuondoa adha ya malazi kwa wageni wanaofika hapa mkoani, pia tutaendelea kuwa walipa kodi halali wa nchi yetu” Mwenyekiti wa Wafanyabiashara Mhe. Njalu Silanga.

Awali akiwasilisha taarifa ya ujenzi wa Hoteli ya Sweet Dreams mtoto wa Mmiliki wa hoteli hiyo, Mary John Sabu amemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka kwa ubunifu na ushawishi wake uliopelekea matukio mengi ya Kitaifa kufanyika mkoani Simiyu, ambayo yamechangia kuongeza mzunguko wa biashara mkoani hapa.

MWISHO

 KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/01/serikali-yawahakikishia-wafanyabiashara.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa