• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Serikali Yatoa Bilioni 1.2 Kulipa Wakulima wa Pamba Simiyu

Posted on: October 20th, 2020

Serikali imetoa jumla ya shilingi bilioni 1.2 kwa ajili ya kukamilisha malipo ya madeni ya wakulima wa pamba kwa msimu wa mwaka 2019 mkoani Simiyu, ambapo kufikia tarehe 21 Oktoba 2020 wakulima wote waliokuwa wanadai fedha watakuwa wameshalipwa fedha zao.

Taarifa hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka jana tarehe 19 Oktoba 2020 katika kikao cha wadau wa pamba kilichofanyika mjini Bariadi kwa lengo la kufanya tathmini ya utekelezaji wa mpango mkakati wa mageuzi ya kilimo cha zao la pamba kwa mwaka 2019/2020 na mpango wa uzalishaji kwa mwaka 2020/2021.

" Tulishafanya uhakiki wa wakulima wetu wote, kufikia Jumatano wakulima wote waliokuwa wanadai malipo ya pamba kwa mwaka 2019 watakuwa wamelipwa fedha zao; vyama vya ushirika hakikisheni kila mkulima anapata fedha yake, ole wenu wakulima walalamike kuwa hawajapaya fedha zao au fedha zao zimekatwa mtakuwa hamjipendi," alisema Mtaka.

Aidha, Mtaka amewakata Maafisa Ushirika wa Halmashauri waandae taarifa ya malipo ya pamba kwa wakulima kwa malipo ya awamu ya kwanza yaliyofanyika Septemba na malipo yanayofanyika sasa ili kupata takwimu za wakulima waliolipwa, kilo zilizolipwa na fedha zilizolipwa kwa kila mkulima ifikapo Oktoba 22, 2020.

Naye Naibu Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe amesisitiza umuhimu wa Vyama vya msingi vya Ushirika (AMCOS) vipatavyo 70 vya mfano kuingia mkataba na makampuni ya ununuzi wa pamba ili Bodi ya pamba itakapotoa leseni za ununuzi wa pamba isitoe leseni kwa wanunuzi wengine kununua katika AMCOS hizo.

“Ninataka hizi AMCOS 70 kwa kupitia Bodi ya pamba, Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Mrajisi wa Vyama vya Ushirika mtambue kampuni ambayo itaingia mikataba na hizi AMCOS moja kwa moja ili Bodi ya pamba itakapotoa leseni isitoe leseni kwa mnunuzi mwingine kwenda kwenye hizo AMCOS,” alisema Bashe.

Katika hatua nyingine Bashe amesema ni vema wakulima wenye mashamba ya pamba yaliyosajiliwa wapewe hati za kimila wapewe hati za kimila ili waweze kukopesheka, huku akitoa wito kwa taasisi za fedha kutoka kwenye mifumo za kizamani ya biashara (utoaji mikopo) ili mifumo ya mikopo iwe na uhusiano wa moja kwa moja na sekta ya kilimo.

Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Pamba, Bw. Marco Mtunga amesema ipo haja kwa wadau wa pamba kuona namna ya kuwasaidia wakulima kuongeza tija katika uzalishaji wa pamba kwa kuwa kumekuwa na dhana kwamba bei ya pamba ndiyo tatizo, ambapo amebainisha kuwa changamoto kubwa katika uzalishaji wa pamba ni tija ndogo.

Mkurugenzi wa Shirika lisilo la Kiserikali la Gatsby Tanzania ambalo limeshiriki kuandaa mkakati wa mageuzi ya uzalishaji wa zao la pamba mkoani Simiyu, Bw. Samwel Kilua amesema kama wadau muhimu wamejipanga kufanikisha mkoa wa Simiyu kuwa mfano wa maeneo mengine yanayozalisha pamba.

Akiwasilisha taarifa ya tathmini ya utekelezaji wa mpango mkakati wa mageuzi ya kilimo cha zao la pamba kwa mwaka 2019/2020 na mpango wa uzalishaji kwa mwaka 2020/2021, Afisa Kilimo wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Bibi. Kija Kayenze amesema katika msimu wa ununuzi wa pamba wa mwaka 2020/2021 unaoendelea hadi kufikia tarehe 04 Oktoba 2020 kilo 111,610,227 zimeshanunuliwa.

Aidha, Kayenze amesema Mkoa wa Simiyu unaongoza kwa kilo 62,822,941 za pamba mbegu ambazo kati yake kilo 4,479,117 ni pamba kilimo hai.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/10/serikali-yatoa-bilioni-12-kulipa.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa