• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Serikali yakubaliana na Wanunuzi Kununua Pamba Shilingi 1200, Yakubali Kufidia Bei ikishuka Soko la Dunia

Posted on: July 19th, 2019

Naibu Waziri wa kilimo, Mhe. Omary Mgumba amesema Serikali imekaa na wanunuzi wa pamba na kwa pamoja wamekubali kuanza rasmi kununua pamba kwa bei elekezi ya shilingi 1200 na ikiwa kutakuwa na hasara watakayopata kutokana na bei ya zao hilo kushuka katika soko la dunia (baada ya Agosti 15,  2019 )Serikali itafidia.

Mhe. Mgumba ameyasema hayo katika nyakati tofauti wakati akiwa kwenye ziara yake ya kukagua mwenendo wa ununuzi wa zao la pamba katika Wilaya ya Bariadi na Maswa Mkoani Simiyu.

Amesema awali wanunuzi wengi walisita kununua pamba kwa bei kubwa na kuuza kwa bei ndogo  kutokana na kushuka kwa bei ya pamba katika soko la dunia, lakini Serikali kwa kuwathamini wakulima, imesema pamba itanunuliwa kwa shilingi 1200 na ikiwa kuna hasara zozote za kibiashara watakazopata wanunuzi baada ya tarehe 15/08/2019 serikali itafidia.

“Tumekubaliana na wanunuzi kuwa waingie rasmi sokoni wanunue kwa bei elekezi ya shilingi 1200 kama kuna kushuka bei au  kutakuwa na hasara yoyote  hayo Serikali itabeba lakini wao waendelee kununua pamba kupitia vyama vya ushirika, msikubali kuuza pamba yenu chini ya bei ya shilingi 1200” alisema Mhe. Mgumba.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bariadi mhe. Festo Kiswaga amesema tayari wanunuzi wawili ambao ni NSAGALI na NGS Company wamepeleka fedha katika Vyama vya ushirika vya Msingi wilayani Bariadi na wanunuzi wengine wanaendelea kwenda kununua.

Nao wakulima waliotembelewa na Mhe. Naibu Waziri wa Kilimo wameiomba Serikali kutoa mbegu, dawa na viuatilifu kwa wakati ili waweze kuongeza tija katika uzalishaji jambo ambalo Mhe. Mgumba alilitolea ufafanuzi kuwa linaendelea kushughulikiwa kwa kusajili wakulima ili kujua idadi kamili ya wakulima na kutoa pembejeo za kutosha kulingana na idadi ya wakulima.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri wa kilimo, Mhe. Omary Mgumba ametoa pole kwa wakulima wa Kijiji cha Shinyanga Mwenge wilayani Maswa kwa naiba ya Serikali kutokana na tatizo walilopata la kuunguliwa na pamba yao katika ghala ya Chama cha Ushirika cha msingi na kuelezwa kusikitishwa sana na tukio hilo.

Akitoa salamu hizo za pole kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amesema Serikali imesikitishwa sana janga hilo na iko pamoja nao, huku akitoa wito kwa wanachama wa Chama cha Ushirika cha Msingi  kuchukua tahadhali ya moto katika maeneo waliyokusanya pamba.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe ametoa wito kwa wanachama wa vyama vya ushirika kuchagua viongozi waadilifu.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/07/serikali-yakubaliana-na-wanunuzi.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa