• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RITA Kuanza Usajili na Kutoa Vyeti vya kuzaliwa kwa Watoto wa Umri chini ya Miaka Mitano Mwezi Machi Mkoani Simiyu

Posted on: February 24th, 2018

Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini hapa nchini (RITA) unatarajia kuanza kutekeleza mpango wa kusajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano kuanzia mwezi Machi ,  mwaka huu mkoani Simiyu.

Hayo yameelezwa na Kaimu Mtendaji Mkuu wa RITA, Bi.Emmy Hudson wakati wa Ufunguzi wa semina ya viongozi ngazi ya Mkoa na wilaya iliyofanyika Mjini Bariadi kwa lengo la kuwapa uelewa wa kina viongozi hao juu ya mpango huu utakaotekelezwa katika maeneo mbalimbali hapa nchini.

Amesema hali ya usajili nchini hairidhishi ambapo amebainisha kuwa, kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 ni asilimia 13.4 tu ya wananchi hapa nchini ndiyo waliosajiliwa na kupewa vyeti vya kuzaliwa.

Ameongeza kuwa ili kuboresha mazingira ya usajili nchini Wakala wa  Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) imeandaa mkakati wa maboresho ya kuhakikisha kuwa kila tukio la uzazi linalotokea nchini linasajiliwa kwa wakati,  ambao pia unalenga makundi matatu la kwanza likiwa ni la watoto chini ya  miaka mitano, kundi la miaka mitano hadi 17 na kundi la miaka 18 na kuendelea.

“Tutakuwa hapa Simiyu kusajili watoto wa umri wa chini ya miaka mitano ambao idadi yao ni 351, 000,  takwimu zinaonesha ni asilimia tano tu ya watoto ndiyo waliosajiliwa, kwa hiyo hali ya usajili na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa Simiyu iko chini na ndiyo maana RITA tumeona tuje ili watoto wote wa Simiyu wapate vyeti vya kuzaliwa na kusajiliwa” alisema Kaimu Mtendaji Mkuu RITA.

Amesema RITA itafanya kampeni kwa muda wa wiki mbili za mwanzo ili kuwaandikisha watoto wote ambao walikuwa hawajaandikishwa na kupewa vyeti vya kuzaliwa, baada ya hapo watoto wote watakaozaliwa baada ya hiyo kampeni wataandikishwa katika Ofisi za Watendaji wa Vijiji, Kata na kwenye vituo vya Tiba ili kusogeza huduma karibu na wananchi.

Aidha, Kaimu mtendaji Mkuu RITA amesema katika kuhakikisha kila mtoto anasajiliwa Serikali imeondoa ada kwa kundi la watoto walio chini ya umri wa miaka mitano hivyo wananchi watapata huduma hii bila malipo yoyote.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amesema watumishi watakaoshiriki zoezi la usajili na utoaji wa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto chini ya miaka mitano hususani Watendaji wa Kata naVijiji wajengewe uwezo na akaziagiza Kamati za Ulinzi na Usalama za Wilaya Mkoani humo  kusimamia zoezi hili ili lifanyike kwa ufanisi mkubwa na uzalendo.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt.Seif Shekalaghe amesema mpango huu wa usajili na kutoa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto chini ya miaka mitano utawasaidia wananchi kupata huduma karibu na maeneo wanayoishi (Ofisi za Watendaji wa Kata na Vijiji) kwa kuwa awali walikuwa wanalazimika kwenda kwenye Ofisi za Wakuu wa Wilaya ili kupata vyeti hivyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi, Ndg.Abdallah Malela amesema viongozi wa Wilaya watahakikisha kila mtoto anayezaliwa anaandikishwa kupitia Ofisi za Watendaji wa Kata na Vijiji na kupewa cheti,  jambo litakalowasaidia kupata takwimu zitakazotumika kufanya maoteo ya wanafunzi wanaopaswa kuanza darasa la kwanza na darasa la awali miaka ijayo.

Kikao hiki kiliwahusisha Wajumbe wa Kamati za Ulinzi na Usalama Mkoa na Wilaya, Makatibu Tawala Wasaidizi wa Sekretarieti ya Mkoa, Maafisa Maendeleo ya Jamii wa Mkoa na Wilaya, Maafisa Ustawi wa Jamii wa Wilaya, Waganga Wakuu wa Wilaya, Waratibu wa Huduma za Afya ya mama  na mtoto pamoja na watumishi wanaoshughulikia usajili wa vyeti vya kuzaliwa katika Ofisi za Wakuu wa Wilaya.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI JUU YA HABARI HII FUNGUA HAPA:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/02/rita-kuanza-usajili-na-kutoa-vyeti-vya.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa