• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka:Tutakuwa na Uwanja wa NaneNane utakaofanya Maonesho ya Kilimo Biashara

Posted on: May 18th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema dhamira ya Kanda mpya ya  Maonesho ya Kilimo na Sherehe za Nane Nane ya Ziwa Mashariki inayojumuisha mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga ni kuwa na Uwanja wa Nanenane utakaofanya  Maonesho ya  Kilimo Biashara.

Mtaka amesema hayo wakati akifungua kikao cha  Maandalizi ya Maonesho ya Nanenane ya Kanda ya Ziwa Mashariki yatakayofanyika katika viwanja vya Nyakabindi kilichowakutanisha Wakuu wa Mikoa mitatu ,Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi Watendaji wa Halmashauri na Sekretarieti za Mikoa hiyo, ambacho kilifanyika mjini Bariadi.

Amesema pamoja na kufanya maonesho ya Kilimo Nanenane ambayo huwa yanafanyika kuanzia Agosti Mosi hadi Agosti 08 kila mwaka,  kutafanyika Maonesho mengine mara nne kwa mwaka pamoja na matukio mengine yatakayofanyika katika uwanja huo ili kuwe na tija kwa  Halmashauri kuwekeza fedha katika uwanja huo.

“Haiwezekani Halmashauri zetu zikawekeza katika uwanja wa NaneNane halafu uwanja uwe unatumika  tarehe 01 hadi 08 mwezi wa nane kila mwaka tu, ni lazima  tuwe na viwanja ambavyo vitafanya maonesho ya kilimo biashara lakini eneo lile ukiacha maonesho haya ya NaneNane tutafanya maonesho mara nne kwa mwaka” alisema.

Ameongeza kuwa ili kuendana na hali ilivyo sasa ni vema Halmashauri zikakubaliana kujenga jengo la maonesho (exhibition hall) na kuwa na maeneo ya nje kwa ajili ya vipando na mifugo kama ilivyopendekezwa katika vikao vya awali,  badala ya kutumia vibanda na mahema kama ilivyozoeleka, ili kuifanya Nane Nane ya Kanda Mpya ya Ziwa Mashariki kuwa ya tofauti.

Katika kikao hicho, Halmashauri 21 za Mikoa ya Mara, Shinyanga na Simiyu zimeagizwa kuwasilisha mchango wa kiasi cha shilingi milioni 20 ndani ya siku saba kwa ajili ya malipo ya awali ya ujenzi wa jengo la maonesho, huku Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima akiwataka Wakurugenzi kutelekeleza agizo hilo.

“.....tumekubaliana kuwa kila Halmashauri itatoa shilingi milioni 20 na hili si jambo la masihara, .....ndani ya siku saba tukitoka hapa kila Mkurugenzi atakuja na hundi yake ya shilingi milioni 20, ili itakapofika Juni Mosi haya mambo yakamilike” alisema Malima.  

Naye Mkuu wa Wilaya ya Tarime, Mhe. Glorius Luoga ametoa wito kwa Wakurugenzi wa Halmashauri zote katika mikoa hiyo kuwa wabunifu katika kuhakikisha fedha za kuwezesha ujenzi wa jengo hilo linalotarajiwa kugharimu jumla ya shilingi bilioni 2.1 zinapatikana.

Hivi karibuni Wizara ya kilimo imetangaza Kanda Mpya ya Maonesho ya Nanenane ijulikanayo kama Kanda ya Ziwa Mashariki, ambayo inajumuisha mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga na Uwanja utakaotumika kwa ajili ya Maonesho hayo uko Eneo la Nyakabindi Mjini Bariadi Mkoani Simiyu, ambapo mwaka 2018 Kanda hiyo itakuwa mwenyeji wa maonesho hayo kitaifa.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA KIUNGANISHI HIKI HAPA:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/05/rc-mtaka-tutakuwa-na-uwanja-wa-nanenane.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa