• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka: Viongozi Tutumie Nguvu nyingi Kujifunza kuliko Kuamua

Posted on: March 12th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa viongozi  kutumia nguvu nyingi kujifunza badala ya kutumia nguvu nyingi kuamua ili wanapofanya maamuzi waamue maamuzi yenye tija kwa maendeleo ya wananchi katika maeneo yao.

Mtaka amesema hayo Machi 11, 2019 Mjini Bariadi katika Mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu,ambao uliwashirikisha viongozi ngazi ya Wilaya na Mkoa.

“Ni vizuri tukatumia nguvu nyingi kujifunza kuliko kuamua kwa sababu kama hutaki kujifunza unataka uamue utaamua hata usiyoyajua, inawezekanaje mtu anateuliwa leo kuwa Mkuu wa Mkoa, Wilaya au Mkurugenzi halafu unakuwa mtaalam wa kila kitu, kilimo wewe, afya wewe, elimu wewe ; unafikiri unaweza kutranform ( kufanya mabadiliko/mapinduzi ya) uchumi wa nani?” alisema Mtaka.

Aidha,  katika kumuenzi Mwalimu Nyerere amewaasa viongozi wenzake waliopewa dhamana na Mhe. Rais kuwatumikia wananchi  kushughulika na masuala yanayohusu maendeleo ya wananchi badala ya kujikita katika mambo yasiyo na tija ikiwemo ugomvi kati yao.

“Tumeaminiwa na Mhe. Rais tukapewa dhamana tuwatumikie Watanzania wenzetu tujishughulishe na masuala ya wananchi tuache mambo yasiyo na tija kwa wananchi; hivi kuna haja gani DC kugombana na DED au RC kugombana na RAS? Kwa nini tumsumbue Mhe. Rais badala ya kuongelea masuala ya maendeleo ya wananchi abaki kuzungumzia mambo ya ugomvi wa viongozi? Alihoji Mtaka

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa  Taasisi ya Mwalimu Nyerere, Bw. Joseph Butiku ametoa wito kwa viongozi kuheshimu Katibu ya Jamhuri ya Muungano waTanzania na kuishi katika misingi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere katika uongozi wao.

Aidha, Butiku ametoa rai kwa viongozi wote wa Serikali kutumia madaraka waliyopewa kwa maslahi ya wananchi na wahakikishe wanawafikia  wananchi mpaka ngazi za chini ili waweze kuwasaidia namna bora ya kutumia shughuli za uzalishaji  wanazozifanya hususani kilimo na mifugo kujikwamua kutoka katika umaskini.

Akitoa mada kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, Mjumbe kutoka Taasisi ya  Mwalimu Nyerere Bw. Gallus Abed amesema katika kuwaletea maendeleo wananchi ni lazima viongozi wajiwekee malengo na kusimamia utekelezaji wa malengo hayo na kuhakikisha wanapima matokeo yake.

Nao baadhi ya Viongozi wa Mkoa wa Simiyu wakichangia hoja katika mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote wamezungumzia mchango wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere na namna wanavyomuenzi Mwalimu Nyerere katika utekelezaji wa shughuli zao za kuwaletea maendeleo wananchi.

“Tunaishukuru Taasisi ya Mwalimu Nyerere kwa namna ambavyo imeamua kutufikia na kuendelea kutuonyesha, kutukumbusha na kuturejesha ili tuishi maisha ya Mwalimu Nyerere ambaye amekuwa mfano wa kuigwa” Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Bw. Jumanne Sagini.

“Serikali ya awamu ya tano imekuwa ikiyaishi maono ya Baba wa Taifa, Mwl.Julius Nyerere, kama unavyoona Mhe. Rais amekuwa akisema na sisi tunaona miradi mikubwa ya maendeleo inatekelezwa kwa fedha zetu za ndani” Mkuu wa Wilaya ya Busega, Mhe. Tano Mwera.

“Tunatekeleza fikra za Mwalimu Nyerere kwa kuanzia hasa  katika utekelezaji wa malengo yaliyoko katika Dira ya Maendeleo ya Taifa ya Miaka Mitano kwenye maeneo yetu” Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Bibi.Suzana Sabuni.

MWISHO

 

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akiteta jambo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere Joseph Butiku  katika Mdahalo wa uongozi na maendeleo yenye tija kwa wote uliondaliwa na Taasisi hiyo kwa viongozi wa Mkoa wa Simiyu, ambao ulifanyika Machi 11, 2019 Mjini Bariadi.

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/03/rc-mtaka-viongozi-tutumie-nguvu-nyingi.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa