• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka: Simiyu sasa Tunajadili Maendeleo ya Wananchi siyo Mauaji ya Vikongwe na Albino

Posted on: October 8th, 2017

Mkoa wa Simiyu kwa sasa haujadili tena masuala ya mauaji ya vikongwe na watu wenye ulemavu wa ngozi(albino) badala yake unajidili maendeleo ya wananchi wa mkoa huo.

Hayo yamesemwa jana na Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Anthony Mtaka wakati wa ufungaji wa Makambi ya Waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato(SDA) yaliyoyofanyika katika Uwanja wa Kidinda mjini Bariadi.

“Miaka hii miwili tumejenga mkoa ambao hatujadili mauaji ya albino, mauaji ya vikongwe, watu kukatwa mapanga, tunajadili Wasukuma Wanyantuzu wanaoenda kwenye maendeleo, ndiyo maana leo mtaona kumejengwa magorofa na nyumba nyingine bora, siyo watu wanaoamini kuwa mtu akiua watu anakuwa tajiri” amesisitiza Mtaka.

Ameongeza kuwa waumini hao wanapaswa kuwa mabalozi katika kufanya mambo ya maendeleo  na wakati huo huo wapinge na kukemea mambo maovu katika jamii na kuwa mfano wa kuigwa kwa watu wengine.

Aidha, ametoa wito kwa waumini hao kuchangamkia fursa za miradi mbalimbali itakayotekelezwa mkoani humo ukiwemo mradi wa kilimo katika Skimu ya Umwagiliaji ya Mwasubuya Wilayani Bariadi, ambapo panakusudiwa kulimwa mpunga kupitia kilimo cha kisasa chenye tija.

Wakati huo huo amewataka waumini hao kuyafanyia kazi na kuyatafsiri kwa vitendo mafundisho waliyopewa wakati wa makambi yakiwemo ya ujasiriamali, ili mwaka 2018 watu watakaoshiriki katika makambi kama hayo waone matokeo ya bidhaa zilizotengenezwa kutokana na ujuzi walioupata mwaka huu.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka ametoa wito kwa waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato na wananchi wote kwa ujumla kuwaombe viongozi wa Serikali hususani Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe.Dkt.John Pombe Magufuli, kwa kuwa anafanya kazi kubwa katika kudhibiti wizi na kutetea rasilimali za nchi hii ili ziwanufaishe Watanzania wote.

“Wapo watu wanauliza ni kwa nini Mhe.Rais aombewe, nawaomba tumuombee Mhe.Rais kwa sababu anafanya kazi kubwa kutetea rasilimali za Watanzania, anafanya maamuzi mazito ambayo yanawaumiza baadhi ya watu ambao wamekuwa wakijinufaisha wao na kuwaumiza wenzao; yanagusa biashara za watu ambao wakati mwingine wangetamani Serikali hii ife hata kesho, ni lazima tumuombee Mhe.Rais” amesema Mtaka.  

Akimshukuru Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka,  Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato wa Southern Nyanza Conference inayojumuisha Mikoa ya Simiyu, Mwanza, Shinyanga na Geita, Mch.Sadock Butoke  amesema, Makambi hayo yamekuwa ya mafanikio kwani pamoja na waumini hao kufundishwa Neno la Mungu, wamefundishwa masomo  ya Afya, Ujasiriamali na kaya na familia ambayo yatawaimarisha kimwili na kiroho.

Naye Mbunge wa Viti Maalum(CCM) Mkoa wa Simiyu, Mhe.Leah Komanya amewashukuru viongozi wa dini kwa kazi kubwa wanayofanya ya kuisaidia Serikali kwa kuwaelekeza waumini wao kufanya mambo mema na kuwa na hofu ya Mungu, hali inayopelekea wananchi wengi kutojihusisha na vitendo viovu.

Makambi ya Waumini wa Kanisa la Waadventisha Wasabato yaliyofungwa rasmi jana Jumamosi na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka yamedumu kwa takribani wiki tatu na yalifunguliwa na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe.Festo Kiswaga.

Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato wa Southern Nyanza Conference inayojumuisha Mikoa ya Simiyu, Mwanza, Shinyanga na Geita, Mch.Sadock Butoke akizungumza na waumini wa Kanisa hilo (hawapo pichani) jana, wakati wa kufunga Makambi yaliyofanyika katika Uwanja wa Kidinda Mjini Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka akiimba (mwenye koti)pamoja na waimbaji wa Kwaya ya Kanisa la Waadventisa Wasabato Kurasini(Kurasini Choir) ya Jijini Dar es Salaam wakati wa kufunga Makambi ya waumini wa Kanisa hilo yaliyofanyika katika Uwanja wa Kidinda Mjini Bariadi.

Mbunge wa Viti Maalum(CCM) Mkoa wa Simiyu, Mhe.Leah Komanya akizungumza na Waumuni wa Kanisa la Waadventista Wasabato (hawapo pichani) jana wakati wa kufunga Makambi ya waumini hao yaliyofanyika katika Uwanja wa Kidinda Mjini Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka(kushoto) akifurahia jambo wakati wa kufunga Makambi ya Waumuni wa Kanisa la Waadventista Wasabato(hawapo pichani) jana,  yaliyofanyika katika Uwanja wa Kidinda Mjini Bariadi; anayefuata, Mwenyekiti wa UWT(CCM) Mkoa wa Simiyu, Katibu Tawala Wilaya ya Bariadi, Albert Rutaihwa na Mbunge wa Viti Maalum(CCM) Mkoa wa Simiyu, Mhe.Leah Komanya.

Baadhi ya Waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka (hayupo pichani) alipozungumza nao jana wakati wa kufunga makambi yao yaliyofanyika katika Uwanja wa Kidinda Mjini Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka(mwenye koti na tai) akiwa katika picha ya pamoja na waimbaji wa Kwaya ya Kurasini SDA mara baada ya kufunga makambi ya Waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato jana,  yaliyofanyika katika Uwanja wa Kidinda Mjini Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka(mwenye  tai ya bluu bahari) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Viongozi wa Mkoa huo, waimbaji wa Kwaya ya Kurasini SDA(wenye sare) na baadhi ya Viongozi wa Kanisa la Waadventista Wasabato Southern Nyanza Conference mara baada ya kufunga makambi ya Waumini wa Kanisa hilo jana yaliyofanyika katika Uwanja wa Kidinda Mjini Bariadi.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe.Anthony Mtaka(mwenye koti na tai) akiagana na waimbaji wa Kwaya ya Kurasini SDA mara baada ya kufunga makambi ya Waumini wa Kanisa la Waadventista Wasabato yaliyofanyika katika Uwanja wa Kidinda Mjini Bariadi.

Vijana wa Pathfinder wakimvisha skafu Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka ikiwa ni ishara ya kumkaribisha kwa ajili ya kufunga makambi ya Waumini wa kanisa la Waadventista Wasabato jana yaliyofanyika katika Uwanja wa Kidinda Mjini Bariadi.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa