• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC MTAKA Awakaribisha Wawekezaji Wazawa kuwekeza Simiyu

Posted on: February 16th, 2017

RC MTAKA Awakaribisha Wawekezaji Wazawa Kuwekeza Simiyu


Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka ametoa wito kwa Wafanyabiashara wazawa kuwekeza katika mkoa huo na kuwahakikishia kuwa Serikali iko tayari kuwaunga mkono.Mtaka amesema hayo katika ufunguzi wa Jukwaa la biashara lililofanyika leo mjini Bariadi, ambalo limeandaliwa na Kampuni ya Magazeti ya Serikali(TSN) ikishirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Amesema fursa takribani 14 zimetangazwa katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo baada ya utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) uliopelekea kuandaliwa kwa Rasimu ya mwongozo wa uwekezaji wa mkoa.

"Tunataka kutransform mkoa wa Simiyu na kuufanya kuwa wa tofauti katika kuelekea  kwenye uchumi wa kati, Tungehitaji kujenga mkoa tofauti na watu wengine waje wajifunze; yapo tuliyoanza kutekeleza na yapo yaliyo kwenye pipeline" alisema.
Mtaka amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote mkoani humo, kutoweka urasimu usio wa lazima kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza katika maeneo yao.Ameongeza kuwa mkoa wa Simiyu umeanzisha mfumo tofauti wa kushirikisha Sekta binafsi katika utekelezaji wa Sera ya Tanzania ya Viwanda ambapo wameanza kwa Halmashauri kuendesha viwanda vidogo kwa ubia na Vikundi vya Vijana; Wilaya ya Meatu(kiwanda cha kusindika maziwa) na Wilaya ya Maswa (Kiwanda cha kutengeneza Chaki).Aidha, pamoja na kuwepo kwa viwanda vidogo  Mtaka amesema Serikali mkoani Simiyu imedhamiria kuwa na viwanda vya kati na vikubwa kwa lengo la kuyaongezea thamani mazao ya kilimo na mifugo.Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, ambaye pia ni Mtaalam wa masuala ya biashara, Profesa Elisante Ole Gabriel amewataka wafanyabiashara kuwa na utamaduni wa kulipa kodi kwa hiari ili biashara zao ziwe endelevu.
Pia Profesa Ole Gabriel ametoa rai kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Simiyu kuzijua vema biashara zao na kufanya biashara hizo kimkakati hususani katika kubuni biashara zinazojibu changamoto za jamii na suala la huduma bora kwa wateja.Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Ndg.Richard Kayombo ametoa wito kwa wafanyabiashara kutunza kumbukumbu za biashara zao ili walipe kodi kulingana mapato yao ili kuiwezesha serikali kupata kodi/mapato stahiki.Naye Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali(TSN) ambao ndiyo waandaaji wa Jukwaa la biashara, Dkt. Jim Yonazi amesema wao wanaamini maendeleo ni Habari, hivyo wako tayari kufanya kazi na mkoa wa Simiyu kwa kuwa viongozi wake wanachukia kasi ndogo katika maendeleo.
"Wakati wengine wanaona Simiyu kama mkoa mpya sisi tunaona fursa, tumeamua kupeleka habari za uwekezaji na maendeleo ya mkoa huu sehemu mbalimbali duniani kupitia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na sasa hivi watu zaidi ya 80,000 wanajua nini kinaendelea hapa" alisema.Jukwaa la biashara mkoani Simiyu limeandaliwa na Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) yaani Habari Leo, Daily News na Spoti Leo kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu. Wadau wengine ni Benki ya Maendeleo(TIB), Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Benki ya NMB na Baraza la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi (NEEC).Jukwaa hilo limewahusisha viongozi wa Mkoa huo ngazi ya Mkoa na Wilaya, wafanyabiashara na wadau mbalimbali wa Maendeleo wa Mkoa huo.
Mkuu wa Mkoa wa Simiyu,Mhe.Anthony Mtaka ametoa wito kwa Wafanyabiashara wazawa kuwekeza katika mkoa huo na kuwahakikishia kuwa Serikali iko tayari kuwaunga mkono.Mtaka amesema hayo katika ufunguzi wa Jukwaa la biashara lililofanyika leo mjini Bariadi, ambalo limeandaliwa na Kampuni ya Magazeti ya Serikali(TSN) ikishirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Amesema fursa takribani 14 zimetangazwa katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo baada ya utafiti uliofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Masuala ya Kiuchumi na Kijamii(ESRF) uliopelekea kuandaliwa kwa Rasimu ya mwongozo wa uwekezaji wa mkoa.

"Tunataka kutransform mkoa wa Simiyu na kuufanya kuwa wa tofauti katika kuelekea  kwenye uchumi wa kati, Tungehitaji kujenga mkoa tofauti na watu wengine waje wajifunze; yapo tuliyoanza kutekeleza na yapo yaliyo kwenye pipeline" alisema.
Mtaka amewataka Wakurugenzi wa Halmashauri zote mkoani humo, kutoweka urasimu usio wa lazima kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza katika maeneo yao.Ameongeza kuwa mkoa wa Simiyu umeanzisha mfumo tofauti wa kushirikisha Sekta binafsi katika utekelezaji wa Sera ya Tanzania ya Viwanda ambapo wameanza kwa Halmashauri kuendesha viwanda vidogo kwa ubia na Vikundi vya Vijana; Wilaya ya Meatu(kiwanda cha kusindika maziwa) na Wilaya ya Maswa (Kiwanda cha kutengeneza Chaki).Aidha, pamoja na kuwepo kwa viwanda vidogo  Mtaka amesema Serikali mkoani Simiyu imedhamiria kuwa na viwanda vya kati na vikubwa kwa lengo la kuyaongezea thamani mazao ya kilimo na mifugo.Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, ambaye pia ni Mtaalam wa masuala ya biashara, Profesa Elisante Ole Gabriel amewataka wafanyabiashara kuwa na utamaduni wa kulipa kodi kwa hiari ili biashara zao ziwe endelevu.
Pia Profesa Ole Gabriel ametoa rai kwa wafanyabiashara wa Mkoa wa Simiyu kuzijua vema biashara zao na kufanya biashara hizo kimkakati hususani katika kubuni biashara zinazojibu changamoto za jamii na suala la huduma bora kwa wateja.Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Ndg.Richard Kayombo ametoa wito kwa wafanyabiashara kutunza kumbukumbu za biashara zao ili walipe kodi kulingana mapato yao ili kuiwezesha serikali kupata kodi/mapato stahiki.Naye Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali(TSN) ambao ndiyo waandaaji wa Jukwaa la biashara, Dkt. Jim Yonazi amesema wao wanaamini maendeleo ni Habari, hivyo wako tayari kufanya kazi na mkoa wa Simiyu kwa kuwa viongozi wake wanachukia kasi ndogo katika maendeleo.
"Wakati wengine wanaona Simiyu kama mkoa mpya sisi tunaona fursa, tumeamua kupeleka habari za uwekezaji na maendeleo ya mkoa huu sehemu mbalimbali duniani kupitia Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na sasa hivi watu zaidi ya 80,000 wanajua nini kinaendelea hapa" alisema.Jukwaa la biashara mkoani Simiyu limeandaliwa na Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN) yaani Habari Leo, Daily News na Spoti Leo kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu. Wadau wengine ni Benki ya Maendeleo(TIB), Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA), Benki ya NMB na Baraza la Uwezeshaji wananchi Kiuchumi (NEEC).Jukwaa hilo limewahusisha viongozi wa Mkoa huo ngazi ya Mkoa na Wilaya, wafanyabiashara na wadau mbalimbali wa Maendeleo wa Mkoa huo.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa