• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka Asema Simiyu imejipanga Kuendesha Biashara Kimkakati

Posted on: January 9th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka amezishauri taassi zinazosimamia masuala ya biashara kuwajengea uwezo wafanyabiashara ikiwa ni pamoja na kuwaelimisha umuhimu wa kusajili kampuni zao hatua itakayowawezesha kuendesha shughuli zao kwa tija.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa kampeni ya kitu bomba inayoendeshwa na kampuni ya simu ya Haloteli mjini Bariadi,Mtaka amesema ili kuwawezesha wafanyabiashara kwenda sambamba na mabadiliko ya teknolojia ni muhimu kuandaa mfumo utakaowatambua kuanzia ngazi ya chini hatua itakayosaidia kufuatilia mienendo yao ya kibiashara ikiwemo kuchangia pato la mkoa na taifa kwa ujumla.

“Nawapongeza sana Halotel kwa hatua hii ya ubunifu mliyotuonyesha, ninaamini  huu ni mwanzo mzuri kwenu wa kubuni huduma nyingine muhimu zitakazowasaidia wafanyabiashara na makundi mengine muhimu katika maeneo mbalimbali”.

“Kwa upande wetu Simiyu, sisi ni miongoni mwa mikoa inayoongoza kwa mifugo mingi nchini halikadalika ni mkoa unaoongoza kwa kilimo cha pamba, hivyo tungefurahi sana endapo Halotel mngekuja na vifurushi vitakavyogusa maeneo hayo ,” alisisitiza Mtaka.

Aidha Mtaka ameishauri kampuni ya simu ya Halotel kuweka utaratibu utakaowawezesha kujitathmini mara kwa mara ili kujua nguvu ya soko lake na mahitaji  ya ziada ya wateja wake hatua itakayoiwezesha kuhimili ushindani na kuwa miongoni mwa kampuni zinazoendesha biashara zake kwa kuzingatia mahitaji ya wateja wake.

Halikadhalika Mhe Mtaka ameiagiza kampuni ya Godtech kuhakikisha inawaelimisha wajasiliamali wadogo mkoani Simiyu umuhimu wa kumiliki na kusajili biashara zao kupitia mfumo rasmi ili waweze kunufaika na fursa mbalimbali.

“ Naendelea kusisitiza Simiyu tumejiandaa kuendesha biashara zetu kimkakati, ili kutekeleza adhma hii kwa vitendo, wafanyabiashara  wetu wataendelea kufanya biashara saa 24, lakini pia ninakuagiza mheshimiwa DC fungeni taa sokoni kuruhusu biashara zifanyike mpaka saa nne usiku”, aliongeza RC Mtaka.

Kwa upande wake balozi wa kapeni ya Kitu bomba ambaye pia ni msanii maarufu wa filamu nchini Jackob Stephen maarufu kama JB ameahidi kuzitangaza kikamilifu fursa zinazopatikana mkoani Simiyu kupitia kampeni hiyo huku akiwataka vijana wenye vipaji kuitumia nafasi hiyo kukuza vipaji vyao.

Uzinduzi wa kampeni hiyo ya Kitu Bomba inayolenga kuwajengea uwezo wananchi katika kupambana na umasikini iliyozinduliwa  mjini Bariadi umehudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara na wadau wa maendeleo.

Mwisho

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa