• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RC Mtaka Aongoza Mamia ya Waombolezaji Mazishi ya Kibaso Aliyekuwa Mwalimu Kwaya ya SDA Kurasini

Posted on: July 1st, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amewaongoza mamia ya waomboleaji kutoka mikoa ya Dar es Salaam, Mara, Mwanza, Simiyu na nchi jirani ya Kenya katika mazishi ya aliyekuwa mwalimu na mwimbaji wa Kwaya ya Kanisa la Wadventista Wasabato (SDA) Kurasini, Mwl.Samson Kibaso ambaye pia ni mtunzi wa wimbo wa Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mazishi hayo yamefanyika Juni 30, 2020 katika Kijiji cha Ingrichini Halmashauri ya Wilaya ya Rorya Mkoani Mara na kuhudhuriwa na viongozi wa Kitaifa wa Kanisa la SDA, Wachungaji kutoka konferensi mbalimbali za Kanisa hilo pamoja na viongozi wa Serikali akiwemo Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI Mhe. Mwita Waitara .

Akizungumza na waombolezaji, Mtaka amesema Mwalimu Samson Kibaso amefanya kazi kubwa ambayo imeacha alama ya utumishi wake si tu katika Kanisa la Waadvenista Wasabato(SDA) bali hata katika madhehebu mengine ambayo amefanya kazi nayo kupitia kazi yake ya utunzi wa nyimbo.

“Yapo maandiko yanasema hubirini kwa sauti ya kuimba, kupitia yeye (Kibaso) ameongoa wengi, amegusa wengi, tuna wachungaji ambao wangeweza kufa ndani ya kanisa wanaofahamika kimataifa lakini wasingetoka watu Kenya wakaja hapa; wote tunajua kuna shida ya kusafiri lakini kuna watu kutoka Kenya wakasema lazima wafike kuona safari ya mwisho ya huyu mtu mwema,” alisema Mtaka.

Aidha, Mtaka amesema atakuwa tayari kushiriki katika mambo ambayo Kanisa litayafanya kwa kumuenzi Mwalimu Samson Kibaso huku akibainisha kuwa heshima aliyopewa Mwalimu Kibaso inabeba taswira ya namna kazi ya Kwaya ya Kurasini inavyopokelewa na watu.

Katika hatua nyingine Mtaka ametoa wito kwa wazazi na walezi katika Halmashauri ya Wilaya ya Rorya kuthamini elimu kwa kuhakikisha wanawapeleka watoto wao shule ili wapate elimu huku akisisitiza kuwa elimu ndiyo inaweza kuwawafanya wakashindana na watu kutoka maeneo mengine.

Akitoa mahubiri kabla ya mazishi ya Mwalimu Kibaso, Askofu wa Kanisa la Waadventista Wasabato(SDA) Jimbo la Kusini mwa Tanzania,  Mch. Mark Malekana amemzungumzia Kibaso kuwa alikuwa na mchango mkubwa kwa kanisa, mtu mnyenyekevu pamoja na kipaji alichokuwa nacho, hivyo akatoa wito kwa waimbaji na walimu wengine kuacha kiburi na kutumia vipaji vyao kwa utukufu wa Mungu.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mhe. Mwita Waitara ametoa pole kwa familia, kwaya ya Kurasini na Kanisa la SDA na kubainisha kuwa anatambua kazi kubwa iliyofanywa na Mwalimu Samson Kibaso hivyo atakuwa tayari kushirikiana na familia, kwaya na kanisa katika kuenzi kazi zake.

Nao wanakwaya wa Kwaya ya SDA Kurasini wamesema wamempoteza, nguli wa muziki, mwalimu mahiri wa uimbaji na rafiki yao, huku wakiahidi kumuenzi kwa kuendelea kumuimbia Mungu ili kupitia uimbaji wao watu waendelee kumuona Mungu.

Mwalimu Samson Kibaso alizaliwa mwaka 1956 na amekuwa mwalimu wa kwaya ya SDA Kurasini tangu mwaka 1985, ambapo pamoja na kuwa mwalimu katika Kwaya ya SDA Kurasini Kibaso pia amefundisha kwaya ya madhehebu mbalimbali kama KKKT, Anglican na Moravian.

Pia alitunga na kufundisha nyimbo za taasisi mbalimbali ikiwemo muhimili wa mahakama pamoja na kutunga wimbo wa jumuiya ya Afrika Mashariki ambao mpaka sasa umekuwa ukiimbwa katika nchi zote zinazounda Jumuiya hiyo.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/07/rc-mtaka-aongoza-mamia-ya-waombolezaji.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa