• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RAS Simiyu Awaasa Viongozi wa Dini, Waganga wa Tiba Asili Kushiriki Kupunguza Vifo vya Wajawazito na Watoto

Posted on: February 27th, 2021

Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bi. Miriam Mmbaga ametoa wito kwa viongozi wa dini na waganga wa tiba asili mkoani Simiyu kushirikiana na Serikali katika juhudi mbalimbali za kupunguza vifo vya wakina mama wajawazito  na watoto vitokanavyo na uzazi.

Mmbaga ameyasema hayo katika kikao chake na viongozi wa dini na waganga wa tiba asili wilayani Itilima, kilichofanyika jana Februari 26, 2021 katika makao makuu ya wilaya hiyo Lagangabilili.

“Sisi kama mkoa tunasema hatutaki kuona mwanamke yeyote anapoteza maisha wakati akijifungua na mtoto akipoteza maisha wakati anazaliwa tunasema waliokufa sasa basi, ni muhimu viongozi wa dini na waganga wa jadi wakashirikiana na Serikali katika kueleimisha jamii juu ya umuhimu wanawake wajawazito  kupata huduma stahiki za afya kwa wakati,  tunajua haya makundi yanakutana na yanawahudumia watu wengi,” alisema Mmbaga.

Aidha, Mmbaga amesema Serikali inatambua mchango na kazi nzuri inayofanywa na viongozi wa dini kupitia kamati za amani huku akisisitiza kamati hizo ziendelee kutekeleza majukumu yake ipasavyo ikiwa ni pamoja na kutatua changamoto mbalimbali zinazokutana na taasisi wanazozisimamia (madhehebu ya dini).

Wakati huo huo Mmbaga ametoa rai kwa waganga wa tiba asili mkoani Simiyu kuchagua viongozi waadilifu watakaowaunganisha pamoja na kuwa msaada kwao katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili ili waweze kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, miongozo, kanuni na taratibu za nchi zilizowekwa.

Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Mhe. Benson Kilangi amewapongeza waganga wa tiba asili kwa kuwa wadau muhimu wa maendeleo katika wilaya hiyo kwa kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa, kutoa chakula kwa ajili ya wanafunzi wanaokuwa katika kambi za kitaaluma; huku akiwaomba waimarishe umoja wao na kuwa na uongozi imara ili waweze kutatua baadhi ya changamoto zinazowakabili.

Mchungaji wa Kanisa la EAGT Lagangabilili ameomba Serikali ione uwezekano wa kuunda chombo kitakachowasaidia viongozi wa dini na waganga wa tiba asili ili makundi hayo yaweze kutekeleza majukumu yao kwa misingi ya sheria, kanuni, taratibu na miongozo inayotolewa na serikali, huku Padri Ivo Komba akitoa wito kwa viongozi wa dini kuwaongoza waumini wao katika imani ya kweli iliyo thabiti mbele za Mwenyezi Mungu.

Kwa upande wake Bw. Tandala Shuri Mganga wa asili kutoka kata ya Nkoma ameomba waganga wa tiba asili washirikiane na viongozi wa dini kufanya kazi kwa kufuata taratibu huku akieleza kuwa baadhi ya waganga wa tiba asili siyo waaminifu wamekuwa wakikiuka taratibu zilizowekwa hivyo akaiomba serikali isisite kuwachukulia hatua waganga wote watakaokwenda kinyume cha sheria zilizopo.

“Tunaomba serikali ishughulike na waganga wahalifu na sisi waganga ndiyo tuwe mstari wa mbele kuwafichua wahalifu hao ili uhalifua wao usituchafue waganga wote, tufuate utaratibu unatakiwa na serikali katika kufanya kazi zetu tusitafute kugombana na serikali,” alisema Tandala Shauri.

Mganga Mkuu wa Wilaya ya Itilima, Dkt. Anold Musiba amesema waganga wote wanapaswa kuomba leseni za kuendesha shughuli zao ili waweze kutambulika kisheria ambapo mpaka sasa jumla ya waganga wa tiba asili 1387 wametambuliwa na Halmashauri ya Wilaya ya Itilima.

Aidha, Dkt. Musiba ametumia fursa hiyo kuwaomba waganga hao kuwaelekeza wakina mama wajawazito, wakina mama wenye watoto wenye utapiamlo mkali na matatizo yote ya lishe kufika katika vituo vya kutolea huduma za afya mapema.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2021/02/ras-simiyu-awaasa-viongozi-wa-dini.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa