• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

RAS Simiyu Asitisha Uamuzi wa DC Kuwataka Watumishi Kuchangia Ununuzi wa Mashine ya Ultrasound Iliyoibiwa Bariadi

Posted on: August 15th, 2019

Uongozi wa Mkoa wa Simiyu kupitia kwa Katibu Tawala wa Mkoa, Bw. Jumanne Sagini umesitisha uamuzi wa Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga, uliotolewa jana Agosti 14, 2019 ambapo watumishi wote 137 wa Hospitali ya Mji wa Bariadi walitakiwa kukatwa mishahara yao kwa ajili ya kuchangia fedha ya kununua mashine ya ULTRASOUND, iliyoibiwa katika wodi ya wazazi hospitalini hapo badala yake ameagiza vyombo vya dola vifanye uchunguzi kubaini aliyeiba mashine hiyo na hatua stahiki zichukuliwe.

Sagini ameyasema hayo leo Agosti 15, 2019 wakati akizungumza na watumishi wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Bariadi katika Ukumbi wa Hospitali hiyo Mjini Bariadi.

Amesema uongozi wa Mkoa umetafakari na kuona kuwa si watumishi wote wa hospitali hiyo wamehusika katika upotevu wa mashine hiyo kwa kuwa wanafanya kazi katika idara tofauti na baadhi yao siku ya tukio hawakuwepo, hivyo ni vema vyombo vya dola vikafanya uchunguzi kubaini waliohusika.

" Uongozi wa Mkoa tunarekebisha baadhi ya hatua zilichukuliwa na Mhe. DC jana, hili jambo haliwezi kuwa la watumishi wote 137, kama Serikali tunavyo vyombo vya dola ambavyo kuna watu wanalipwa mishahara kwa kazi hizo za kiuchunguzi, tunataka kifaa hicho kirejeshwe, vyombo hivi vifanye uchunguzi, vichukue hatua kwa watakaobainika ikiwemo kupelekwa mahakamani" amesema.

Katika hatua nyingine Sagini amewataka watumishi wa Hospitali ya Mji wa Bariadi kuimarisha mfumo wa makabidhiano ya kazi na vifaa vya kazi ili kuwepo na taarifa sahihi za wagonjwa na vifaa tiba kama utaratibu unavyotaka.

Kwa upande wao watumishi wa Halmashauri ya Mji wa Bariadi wamewashukuru viongozi wa Mkoa wa Simiyu kwa kusitisha uamuzi wa awali ambao ungewaathiri kiuchumi na kupunguza ari ya kufanya kazi hususani wale ambao hawajahusika na upotevu wa mashine hiyo.

" Tunamshukuru sana kiongozi wetu kwa msamaha aliotutolea kwa sababu tangu jana tumelala kwa presha baada ya kuambiwa kuwa kila mtu alip, mimi uwezo wangu mdogo na mshahara wangu ni mdogo nilikuwa sioni pesa ya kulipa hicho kifaa;namshukuru Mungu kwa uamuzi wa viongozi wa mkoa yaani naongea kwa uchungu mpaka nasikia kulia kwa furaha niliyonayo" amesema Frola Katoyo Mtumishi katika idara ya dawa.

"Nimepokea vizuri uamuzi uliofanywa na viongozi wetu wa mkoa kwa sababu maanuzi yaliyotolewa jana kiuhalisia si kila mtumishi alipaswa kuhusishwa kwenye hili, maana wengine walikuwa likizo, wengine hawakuwepo kazini, hivyo ni sahihi kabisa kuviachia vyombo vya dola; nina uhakikia kuanzia leo watu watafanya kazi maana jana utendaji kazi ulipungua baada ya kupata tu taarifa kuwa wanapaswa kuchangia" alisema Simon Chisomeko Afisa Afya.

Kwa upande wake Katibu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali Kuu na Afya (TUGHE) Mkoa wa Simiyu, Bi. Catherine Nyingi amesema Chama hicho kinaushukuru uongozi wa mkoa kwa kutambua sheria, kanuni na taratibu za Utumishi wa Umma na wameiomba Serikali iendelee kuwa macho katika kusimamia sheria, kanuni na taratibu.

Mashine ya kupima magonjwa ya ndani ya mwili wa Binadamu (ULTRASOUND MACHINE) iliripotiwa kuibiwa katika Wodi ya wazazi katika Hospitali ya Mji wa Bariadi Agosti 05, 2019 na jana Agosti 14, 2019 Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Mhe. Festo Kiswaga akaagiza watumishi wote 137 wa Hospitali hiyo wakatwe fedha kwenye mishahara yao ili mashine hiyo iliyoibiwa inunuliwe.

MWISHO

 KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/08/ras-simiyu-asitisha-uamuzi-wa-dc.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa