• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

VIONGOZI NA WATUMISHI SHIRIKIANENI NA WADAU KUBORESHAJI HUDUMA ZA AFYA

Posted on: March 24th, 2017

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg. Jumanne Sagini  ametoa wito  kwa viongozi na watumishi mkoani humo kushirikiana na wadau mbalimbali wenye nia njema ya kuunga mkono juhudi za Serikali katika uboreshaji wa huduma za afya kwa wananchi.

Sagini ameyasema hayo leo katika ufunguzi wa kikao cha kuutambulisha Mradi wa USAID Boresha Afya, kilichofanyika katika Ukumbi wa Kanisa Katoliki Mjini Bariadi.

Amesema Simiyu ni miongoni mwa mikoa saba ambayo Mradi wa USAID Boresha Afya utatekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano (2017-2022), hivyo akawataka viongozi na wataalam kushirikiana na wadau hao kuhakikisha mradi huu unasaidia kubadilisha mfumo wa utoaji huduma za afya katika maeneo yaliyobainishwa. 

Aidha, amengeza kuwa ujio wa Mradi huu katika Halmashauri zote za Mkoa wa Simiyu uwe ni chachu ya kuhakikisha huduma za Afya zinapatikana kirahisi kwa wananchi wa Mkoa huo.

“Ndugu washiriki nichukue nafasi hii kushukuru mashirika na wadau mbalimbali wanaounga mkono juhudi za Serikali, natoa wito kwa Idara ya Afya Mkoa na wilaya kutoa ushirikiano wa karibu kuhakikisha mradi huu unafanikiwa na unatoa matunda tarajiwa”

Sagini amesema Serikali inafanya juhudi za kukabiliana na viashiria muhimu visivyoridhisha vya Afya ya Uzazi na mtoto ikiwemo kupunguza vifo vya akina mama vitokanavyo na uzazi ambavyo vinafikia 556 kwa kila vizazi hai 100,000 kwa sasa.

“Vifo hivi vinachangiwa na mambo mengi, ikiwemo mahudhurio hafifu ya wajawazito kliniki katika theluthi ya kwanza ya mimba kwa asilimia 24 na wajawazito wanaohudhuria kliniki kwa mahudhurio manne au zaidi kwa asilimia 51” amesema Sagini

Sagini amesisitiza kuwa mafanikio katika suala la kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi halitatatuliwa na sekta ya Afya pekee bali kwa ushirikiano wa sekta zote za maendeleo

Kwa upande wake Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Mkoa wa Simiyu, Dkt.Fredrick Mlekwa amesema Mradi huu umekuja katika wakati muafaka ambao mkoa huo unafanya jitihada mbalimbali za kukabiliana na vifo vya akina mama vitokanavyo na uzazi na vifo vya watoto wadogo chini ya miaka mitano.

Naye Dkt.Joseph Masenga kutoka USAID Boresha Afya amesema mradi huo katika mkoa wa Simiyu utajikita katika kuunga mkono juhudi za Serikali katika huduma za uzazi wa mpango, Malaria, Huduma za Afya ya Mtoto, huduma za Uzazi, Lishe na maeneo mengine mtambuka ikiwemo jinsia, heshima na ushirikishwaji wa jamii katika huduma za Afya (ngazi ya jamii).

Kwa upande wake Mratibu wa Mradi wa USAID Boresha Afya wa Mkoa wa Simiyu , Dkt. Charles Suka amesema utambulisho wa mradi huo umefanyika kwa viongozi na watendaji wa mkoa huo ili wawena uelewa wa pamoja ili waweze kutoa mchango katika utengeenzaji wa mapango mkakati wa kupunguza vifo vya mama na mtoto na kuweka mpango wa utekelzaji wa  wa mradi kwa miaka mitano.

Mradi wa USAID Boresha Afya Mkoani Simiyu, unatekelezwa kwa ubia wa mashirika ya Jhpiego, Engenderhealth katika mikoa ya Kanda ya Ziwa na Magharibi ambayo ni Simiyu, Mara,Kagera, Kigoma, Shinyanga, Geita na Mwanza katika kipindi cha miaka mitano(2017-2022).

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa