• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

NEC Yataka Vyama ya Siasa, Wananchi Kufuata Sheria kuelekea Uchaguzi Mkuu

Posted on: October 1st, 2020

Vyama vya Siasa, wagombea na wananchi wamekumbushwa kuendelea kufuata sheria za nchi katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu kwani sheria hazijasimama hivyo wajihadhari na vitendo vinavyoweza kusababisha vurugu kwa kisingizio cha uchaguzi.

Hayo yamebainishwa jana na Mkurugenzi msaidizi wa huduma za sheria kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi nchini (NEC),Bw. Baraka Leonard wakati akisoma hotuba ya Mwenyekiti wa tume hiyo kwenye ufunguzi wa mkutano wa wadau wa uchaguzi uliofanyika katika ukumbi wa uliopo kwenye jengo la ofisi ya mkuu wa mkoa wa Simiyu mjini Bariadi.

"niwahakikishie wananchi tume ya uchaguzi imejipanga kusimamia uchaguzi mkuu Oktoba ,2020 kwa kufuata katiba, sheria na miongozo iliyopo na tuna Imani kila mdau atatimiza wajibu wake katika hili " alisema na kuongeza kuwa:

"nivitake vyama vya saisa na wagombea kuzingatia maadili ya uchaguzi katika kampeni zao ikiwemo kuepuka lugha za kashfa na maneno ya uchochezi, kuepuka kufanya kampeni zinazoashiria ubaguzi katika misingi ya jinsi, ulemavu, ukabila, udini, maumbile na rangi" aliongeza.

Mbali na hayo aliwatoa hofu wapiga kura wote wenye mahitaji maalumu kwani tayari maelekezo yametolewa kwa watendaji wa uchaguzi kwa kutoa kipaumbele kwa wenye ulemavu, wajawazito, akina mama wanaonyonyesha ,waliokwenda na watoto vituoni, wazee na wagonjwa huku akiongeza kuwa kila mwenye sifa ya kupiga kura ajitokeze na kadi yake kupiga kura katika kituo alichojiandikisha ili kutimiza haki yake ya msingi ya kikatiba.

Kwa upande wake afisa elimu ya mpiga kura kutoka NEC Nuru Riwa alisema tume hiyo itaandaa jalada la nuka nundu (tactile ballot folder) kwa kila kituo cha kupigia kura kwa ajili ya wasiiona ,wenye huku wenye ulemavu wa miguu kituturi kimetengenezwa lengo likiwa kuwapa nafasi na wenye ulemavu kupiga kura.

Riwa aliongeza kuwa upigaji kura utafanyika katika vituo 80,155 na jumla ya watendaji wa vituo 320,620 watasimamia na kuendesha zoezi la upigaji kura vituoni hapo.

Awali mjumbe kutoka shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) mkoa wa Simiyu Alex Benson aliiomba tume kuweka mazingira rafiki kwa viziwi ili kundi hilo liweze kushiriki kikamilifu kwenye uchaguzi huo huku akitolea mfano wawepo wataalam wa lugha ya alama kwenye vituo na kundi hilo liitwe kwa umoja wao kupewa elimu kwani elimu inayotolewa kwanjia nyingine ikiwemo matangazo yanayotumia vipaza sauti hayawafikii.

Akichangia kwenye mkutano wa wadau hao Semeni Kingi ambaye ni mwakilishi wa kundi la wenye ualbino aliiomba tume ya taifa ya uchaguzi kuhakikisha majina ya wagombea wa nafasi za urais, ubunge na udiwani yanaandikwa kwa herufi kubwa kwenye karatasi za kupigia kura ili kuwarahisishia wenye uoni hafifu kusoma kiurahisi.

MWISHO.

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/10/nec-yawataka-vyama-vya-siasa-wananchi.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa