• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Naibu Waziri wa Fedha Atoa Wito kwa Halmashauri Nchini Kubuni Miradi ya Kimkakati

Posted on: June 24th, 2018

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ametoa wito kwa Halamshauri zote nchini kubuni miradi ya kimkakati ya itakayoziongezea mapato badala ya kuendelea kutegemea ushuru na tozo mbalimbali kutoka kwa wananchi.

Dkt. Kijaji amayasema hayo wakati alipotembelea kiwanda cha kutengeneza chaki cha wilaya ya Maswa wakati wa ziara yake ya kujionea utekelezaji wa Sera ya Tanzania ya Vwanda Mkoani Simiyu akiwa na viongozi wa Halmashauri na Chama cha Mapinduzi Wilaya ya Kondoa.

Amesema Dhamira  ya Serikali ni kuhakikisha Halmashauri zote zinabuni miradi ya kimkakati ambayo itaziongezea mapato na akatoa wito kwa Halmashauri zote nchini kujifunza kwa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa ambayo imetengewa shilingi bilioni 8.2 na Serikali kwa ajili ya kutekeleza miradi miwili ya upanuzi wa Kiwanda cha Chaki na kujenga kiwanda cha vifungashio.

“Niwapongeze Simiyu mnafanya kazi nzuri, tunataka kuondoka kwenye ule ukawaida wa Halmashauri zetu kulalamika kuwa Serikali Kuu imechukua vyanzo vya mapato, Serikali Kuu haijachukua kinachohitajika ni ubunifu wa miradi kama Halmashauri ya Maswa ilivyofanya, nitoe wito kwa Halmashaui zote kubuni miradi, Serikali ipo tayari fedha zipo kwa ajili ya miradi ya kimkakati ya kuongeza mapato ya Halmashauri” alisema

 Mbunge wa Maswa Mashariki na Naibu Waziri wa Madini Mhe Stanslaus Nyongo ameiomba Serikali kutoa fedha hizo shilingi Bilioni 8.2 zilizotengwa kwa wakati ili Miradi iliyokusudiwa ya upanuzi wa kiwanda cha chaki na ujenzi wa kiwanda cha vifungashio iweze kutekelezwa kwa wakati.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu amesema katika kukiongezea kiwanda cha chaki uwezo wa  uzalishaji, Halmashauri ya Maswa imenunua eneo ambapo malighafi ya kutengenezea chaki inapatikana, katika Mkoa wa Singida.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa Dkt. Fredrick Sagamiko amesema Halmashauri hiyo imedhamiria kufikisha zaidi ya asilimia 75 ya mapato ya ndani yatakayotokana na viwanda vilivyopo na vinavyoendelea kujengwa wilayani humo.

Awali Dkt. Ashatu alitembelea eneo maalum lililotengwa kwa ajili ya uwekezaji katika viwanda la Halmashauri ya Wilaya ya Maswa mahali ambapo patajengwa kiwanda kikubwa cha kutengeneza chak(upanuzi wa hiki kilichopo) na kujenga kiwanda cha vifungashio

MWISHO

Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredrick Sagamiko akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji alipotembelea kiwanda cha Chaki wilayani Maswa mkoani Simiyu ambapo aliongozana na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa na CCM wilaya ya Kondoa kwa lengo la kujifunza utekelezaji wa sera ya viwanda mkoani humo.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (wa pili kulia)akiangalia viatu vya ngozi vinavyotengenezwa katika kiwanda cha Senani wilayani Maswa mkoani Simiyu baada ya kutembelea kiwanda cha Chaki wilayani Maswa akiwa na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa na CCM wilaya ya Kondoa kwa lengo la kujifunza utekelezaji wa sera ya viwanda

Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akimkabidhi Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji chupa ya maziwa ya Meatu wakati wa ziara yake mkoani humo akiwa na viongozi wa Halmashauri ya Kondoa na viongozi wa CCM wilaya ya Kondoa mkoani humo kwa ajili ya kujifunza utekelezaji wa Sera ya Tanzania ya Viwanda mkoani humo.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akisaini ubao kwa kutumia chaki za Maswa katika kiwanda cha chaki Maswa mkoani Simiyu, baada ya kutembelea kiwanda hicho akiwa na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa na CCM wilaya ya Kondoa kwa lengo la kujifunza utekelezaji wa sera ya viwanda mkoani humo.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akionesha risiti ya EFD baada ya kununua chaki za Maswa mkoani Simiyu, baada ya kutembelea kiwanda cha chaki akiwa na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa na CCM wilaya ya Kondoa kwa lengo la kujifunza mkoa wa Simiyuunavyotekeleza sera ya viwanda.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akiwa katika picha ya pamoja na vijana wa Kiwanda cha Maswa(waliochuchumaa), viongozi mbalimbali wa mkoa wa Simiyu kutembelea kiwanda cha Chaki wilayani Maswa akiwa na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa na CCM wilaya ya Kondoa kwa lengo la kujifunza mkoa wa Simiyu unavyotekeleza sera ya viwanda.

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akisaini ubao kwa kutumia chaki za Maswa katika kiwanda cha chaki Maswa mkoani Simiyu, baada ya kutembelea kiwanda hicho akiwa na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa na CCM wilaya ya Kondoa kwa lengo la kujifunza mkoa wa Simiyu unavyotekeleza sera ya viwanda.

Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akimkabidhi Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa chupa ya maziwa ya Meatu wakati ziara ya Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Ashatu Kijaji na viongozi wa Halmashauri hiyo na viongozi wa CCM wilaya ya Kondoa mkoani Simiyu kwa ajili ya kujifunza mkoa wa Simiyu unavyotekeleza Sera ya Tanzania ya Viwanda.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka akitoa maelezo kwa Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji alipotembelea eneo la uwekezaji wa viwanda wilayani Maswa ambapo aliongozana na Viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa na CCM wilaya ya Kondoa kwa lengo la kujifunza utekelezaji wa sera ya viwanda mkoani humo.

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa