• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Naibu Waziri Mabula Atoa Wito Wananchi Simiyu Kuchangamkia Fursa ya Nyumba za Shirika La Nyumba

Posted on: October 27th, 2018

Naibu waziri wa ardhi ,nyumba na maendeleo ya makazi Mhe.Angelina Mabula ametoa wito kwa wakazi wa mkoa wa SIMIYU kutumia fursa za nyumba za makazi zinazotarajiwa kujengwa katika eneo la Isanga Mjini Bariadi na Shirika la Nyumba la Taifa

Wito huo ameutoa mkoani Simiyu alipokutana na wadau mbalimbali katika kongamano la ujenzi wa nyumba za makazi mkoani Simiyu lililohudhuriwa na viongozi wa serikali mkoani humo wakiongozwa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya mkoa mkoa wa Simiyu,wakuu wa wilaya wakurugenzi, makatibu tawala wilaya, wakuu wa idara na watumishi wa kada mbalimbali kutoka halmashauri zote, wafanyabiashara na viongozi wa vyama vya wafanyakazi lengo likiwa ni kuangalia aina ya nyumba zitakazojengwa na Wateja watarajiwa.

Mabula amesema azma ya wizara ya ardhi ,nyumba na maendeleo ya makazi ni kumwezesha kila mtanzania kunufaika na nyumba zinazojengwa na shirika hilo, huku akisisitiza Taasisi nyingine zinazohusika na uwekaji wa miundombinu muhimu kuanza utaratibu wa kuweka miundombinu hiyo ili kuwapunguzia gharama wanunuzi.

“ Tunatarajia taasisi zinazohusika ziwe zimeshaanza kupeleka huduma huko, wakati NHC wanaanza kujenga nyumba zao pale gharama itakuwa iko chini kwa sababu hivi vitu vingine vitakuwa vimewekwa na taasisi nyingine na kazi yao itakuwa ni kurudiisha fedha zao kupitia bili za umeme, maji”

“Awali nyumba za NHC zilikuwa zikilalamikiwa kuwa ni za gharama kubwa kutokana na wao kufanya kazi zote wao wenyewe, ujenzi wa nyumba na uwekaji wa miundombinu ya maji , umeme, barabara, viwanja vya michezo na huduma nyingine, lakini tunamshukuru Mhe. Rais alishatoa maelekezo kwa wizara na mamlaka husika kuhakikisha wanaweka miundombinu ya huduma zote muhimu mahali ambapo NHC wanajenga nyumba zao” alisema.

Wakitoa maoni yao baadhi ya wadau wametoa ushauri kwa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kuona namna ya kujenga nyumba zenye gharama nafuu zaidi ili wananchi wengi hususani wale wenye kipato cha chini waweze kunufaika na mradi huu.

“Ninaiomba Serikali kuangalia upya gharama za nyumba za makazi zinazojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa(NHC) ili kuwawezesha watumishi na wananchi wengi kumudu gharama za kununua nyumba hizo kwa kuwa wengi ni wenye vipato vya chini, pia benki zinazowakopesha wananchi wanaonunua nyumba hizo zitoe mikopo kwa masharti ambayo hayatawaumiza wakopaji” alisema Mbunge wa Itilima, Mhe. Njalu Silanga.

“Ninashauri Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) kuona haja ya kuwa na mpango mkakati wa kuboresha makazi ya wakulima ambao wamejiunga na Vyama vya Ushirika vya Msingi(AMCOS) ili vyama hivyo, benki pamoja na NHC waje namna   kujenga nyumba zenye bei nafuu zaidi na kundi kubwa zaidi liweze kunufaika” alisema Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredrick Sagamiko.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe.Anthony Mtaka amelipongeza Shirika la Nyumba la Taifa kwa kuwa chachu ya Maendeleo ya makazi bora nchini, huku akibainisha kuwa Shirika hilo linaweza kuona namna ya kufanya kazi na Halmashauri mkoani humo katika kukabiliana na changamoto ya makazi kwa watumishi.

Wakizungumza katika Kongamano hilo Wawakilishi wa taasisi za fedha zikiwemo Benki za NMB, CRDB na Azania Bank  wamesema wamejipanga katika utoaji wa mikopo ya nyumba kwa wale walio tayari na wenye vigezo vinavyotakiwa.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/10/naibu-waziri-mabula-atoa-wito-wananchi.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa