Mwenge wa Uhuru 2017 umehitimisha Mbio zake Mkoani Simiyu na kukabidhiwa katika Mkoa wa Shinyanga leo tarehe 10/07/2017.
Akikabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Katibu Tawala Mkoa wa Shinyanga, Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Ndg.Jumanne Sagini amesema Mwenge wa Uhuru umekimbizwa katika Halmashauri zote sita za Mkoa huo katika umbali wa kilometa 780.
Sagini amesema Mwenge wa Uhuru ukiwa Mkoani Simiyu umeweza kuweka mawe ya msingi, kufungua, kuzindua, kukagua na kuona jumla ya miradi 43 ya maendeleo yenye thamani ya shilingi 8,450,841,622/= ambazo ni fedha kutoka Serikali Kuu, Halmashauri, nguvu za wananchi,sekta binafsi na washirika wa maendeleo.
Mbio za Mwenge wa Uhuru mwaka 2017 zimebeba Ujumbe Mkuu “SHIRIKI KATIKA KUKUZA UCHUMI WA VIWANDA KWA MAENDELEO YA NCHI YETU”
Bariadi - Somanda
Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.
Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054
Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054
Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz
Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa