• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Mkuu wa JKT Afanya Ziara Simiyu Kukagua Miradi Inayotekelezwa na SUMA JKT

Posted on: July 4th, 2020

Mkuu wa JKT nchini Meja Jenerali Charles Mbuge wamefanya ziara ya siku moja mkoani Simiyu kwa lengo la kukagua maendeleo ya utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na Shirika la Uzalishaji Mali la Jeshi hilo SUMA JKT.

Akikagua miradi hiyo jana Julai 03, 2020 Meja Jenerali Mbuge amewataka wasimamizi wa miradi hiyo kuongeza kasi katika utekeleza ili miradi hiyo iweze kukamilika kwa wakati.

“Nataka site (maeneo ya kazi) zichangamke, hakikisheni mnaongeza watenda kazi wakiwemo mafundi na vibarua; tafuteni mashine zenye uwezo wa kufyatua tofali nyingi kwa wakati mmoja ili kazi iende kwa kasi na viwango," alisema Mbuge.

Aidha, Brigedia Jenerali Mbuge amewaagiza viongozi wote wanaosimamia utekelezaji wa miradi hiyo kuhakikisha kuwa wanafanya kazi bila kusimamiwa huku akisisitiza kuwa atafuatilia utekelezaji wa maagizo yote aliyoyatoa kwa viongozi wa JKT ambao ni wasimamizi wa miradi hiyo.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Serikali ya Mkoa inatambua kazi nzuri inayofanywa na SUMA JKT mkoani hapa, huku akibainisha kuwa anatarajia kuona matokeo zaidi baada ya ziara ya Mkuu wa JKT kutokana na maelekezo aliyotoa kwa wasaidizi wake ambayo mengine amehusika moja kwa moja kuwa sehemu kubwa ya utatuzi wa changamoto kwenye miradi hiyo.

"Ziara hii imekuwa ziara darasa na sisi kama viongozi tumejifunza mengi kwako Mkuu wa JKT hasa katika suala la kufanya maamuzi; tunategemea kuona matokeo baada ya ziara hii kutokana na maelekezo uliyoyatoa," alisema Mtaka.

Naye Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Donatus Weginah amesema Serikali ya Mkoa na taasisi za Umma zilizopo inaunga mkono SUMA JKT huku akiomba zaidi ya shilingi milioni 700 zilizolipwa kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Simiyu zitumike kufanya kazi hiyo ili kutoa nafasi kwa Katibu Tawala Mkoa kupewa fedha nyingine na lengo la kukamilisha jengo hilo Desemba 2020 litimie.

Msimamizi Mkuu wa SUMA JKT Kanda ya Ziwa, Kapteni Fabian Buberwa ameahidi kutekeleza maelekezo yote yaliyotolewa na Mkuu wa JKT na kusisitiza kuaysimamia kwa kadri alivyoelekeza.

SUMA JKT katika Mkoa wa Simiyu inatekeleza ujenzi wa miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa jengo la wodi ya wazazi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa, Jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa , ujenzi wa jengo la wizara ya kilimo katika uwanja wa nanenane Nyakabindi, ujenzi wa kiwanda cha chaki na kiwanda cha vifungashio.

MWISHO.

 KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2020/07/mkuu-wa-jkt-afanya-ziara-simiyu-kukagua.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa