• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Mkurugenzi wa TANTRADE atoa Wito kwa Makampuni, Wafanyabiashara, Wakulima Kujiandaa NaneNane mwaka 2018 Kanda ya Ziwa Mashariki

Posted on: April 12th, 2018

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara (TanTrade ) Edwin Rutageruka ametoa wito kwa wakulima,wafanyabiashara na makampuni madogo Nchini kujiandaa na kushiriki maonesho ya Kilimo na Sikukuu ya Wakulima NaneNane ya Kanda ya Ziwa Mashariki ili kujifunza teknolojia mpya kutoka katika makampuni ya nje.

Maonesho hayo ambayo mwaka 2018 yanatarajia kufanyika kitaifa Mkoani Simiyu yameelezwa kuwa yatakuwa ya kipekee ikilinganishwa na miaka mingine huku yakitoa fursa zaidi kwa wafanyabiashara na makampuni madogo kujitokeza kwa wingi kushiriki.

Akizungumza leo Aprili 12  katika kikao cha maandalizi ya Nane Nane Kitaifa yanayotarajiwa kufanyika Mkoani Simiyu, Mkurugenzi Mkuu wa TanTrade Edwin Rutageruka amesema kuwa taasisi yake iko tayari kutoa ushirikiano wa dhati kwa uongozi wa Mkoa wa Simiyu ili kuhakikisha wanayafanya maonesho hayo kuwa ya kipekee.

Amesema ni vema makampuni madogo, wakulima na wafanyabiashara wakajitokeza kushiriki maonesho hayo kwani watapata fursa ya kujifunza Teknolojia mpya kutoka nchi za nje ambazo zitashiriki maonesho hayo.

“Ni vema Wafanyabiashara, wakulima na makampuni madogo yakajitokeza kushiriki maonesho hayo kwani tumejipanga vizuri, tumetenga maeneo mazuri na tutapanga kulingana na sekta mbalimbali ”alisema

Ameongeza kuwa katika kuyatangaza maonesho hayo ya Nane Nane ya mwaka huu 2018 , TanTrade itaandaa dawati maalum la kuutangaza rasmi Mkoa wa Simiyu na fursa zilizopo ili Watanzania na Wawekezaji wajitokeze kwa wingi kuwekeza.

Aidha,  Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Anthony Mtaka amesema uwepo wa Maonesho ya Nane Nane Kanda ya Ziwa Mashariki yatakayofanyika Mkoani humo, kwa kushirikiana na  Mikoa ya Mara na Shinyanga ambayo kwa pamoja inaunda Kanda hiyo, yatasaidia wakulima kujifunza kwa washiriki kutoka maeneo mbalimbali na hatimaye kuongeza thamani ya mazao yao.

Mtaka ameeleza kuwa mbali na Uwanja wa Maonesho kutumika kwa ajili ya Maonesho ya Sikukuu ya Wakulima Nane Nane, Uwanja huo utatumika katika shughuli mbalimbali za kiuchumi ambazo zitawanufaisha kiuchumi wananchi na Taifa kwa ujumla.

Akizungumza kwa niaba ya Wafanyabiashara wa Mkoa wa Simiyu, Bw. Bahini Masunga amesema kuwepo kwa Maonesho ya Nane Nane kutawasaidia Wafanyabiashara na wananchi kwa ujumla  kutambua fursa mbalimbali pamoja na kujiongezea ujuzi wa namna ya kuongeza thamani katika bidhaa zao.

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI KUHUSU HABARI HII FUNGUA HAPA:-https://simiyuregion.blogspot.com/2018/04/mkurugenzi-tantrade-atoa-wito-kwa.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa