• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Mjumbe wa NEC Gachuma Awaongoza Wananchi, Viongozi Simiyu Mazishi ya DC na Mbunge Mstaafu, Katibu Mwenezi CCM Mkoa Danhi Makanga

Posted on: June 27th, 2018

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa kupitia Mkoa wa Mara, Christopher Gachuma amewaongoza wananchi na viongozi wa CCM na Serikali wa mkoa wa Simiyu katika mazishi ya aliyewahi kuwa mbunge wa Bariadi Mashariki , Mkuu wa Wilaya katika maeneo mbalimbali hapa nchini,ambaye pia alikuwa Katibu wa Itikadi  na Uenezi wa CCM Mkoa wa Simiyu, Bw. Danhi Makanga, ambayo yamefanyika katika Mtaa wa  Kidulya Mjini Bariadi .

Akizungumza kwa niaba ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi Taifa, Gachuma ametoa pole kwa familia, ndugu na jamaa wote walioguswa na msiba huo, huku akiwaasa ndugu na familia kuendelea kuishi maisha ya umoja na kushirikiana.

Aidha, Gachuma amepongeza mkoa wa Simiyu kwa ushirikiano uliopo kati ya Viongozi wa Chama na Serikali katika masuala yote ikiwa ni pamoja na misiba na akikiri kuwa yeye pamoja na baadhi ya viongozi wa mkoa wake(Mara) walioongozana naye wamejifunza jambo hilo kutoka Simiyu.

"Napenda niupongeze uongozi wa mkoa wa Simiyu kwa namna mnavyoshirikiana, msiba wa ndugu yetu Makanga mmeubeba wote kwa pamoja tumeona kuna umoja na ushirikiano kati ya viongozi wa Chama na Serikali hili ni jambo jema sana , bahati nzuri nimefuatana na Katibu Mwenezi wangu wa Mkoa utaratibu huu na sisi tunaubeba kama somo" alisema Gachuma.

Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Simiyu, Mhe. Enock Yakobo akitoa salamu za rambirambi ametoa pole kwa familia na kuwaomba ndugu na familia waendelee kuwa wamoja na wasikubali kugawanywa kwa namna yoyote, huku akielezea kuwa CCM imempoteza mtu muhimu makini sana ambaye alikuwa na mchango mkubwa katika Chama, Serikali na Taifa kwa ujumla.

Mhe. Yakobo amewashukuru viongozi wa CCM Taifa kwa kutuma mwakilishi, pia akawashukuru wananchi, viongozi wa Chama na Serikali mkoani Simiyu kwa namna walivyoonesha umoja na ushirikiano katika msiba wa Bw. Danni Makanga hali ambayo imeleta heshima kwa Chama na kumfanya marehemu Makanga kuzikwa kwa heshima kama kiongozi wa Chama.

Akimzungumzia marehemu Danni Makanga, Mkurugenzi wa Shirika la Reli Tanzania, Masanja Kadogosa amesema tangu marehemu akiwa Mbunge wa Bariadi na Mkuu wa Wilaya katika maeneo mbalimbali na kubainisha kuwa alikuwa kiongozi ambaye kupitia yeye vijana wa sasa wanaweza kujifunza namna ya kuitumikia Serikali na wananchi kupitia yeye.

Naye Mkuu wa Wilaya mstaafu, Malietha Sanka  ambaye alifanya kazi na marehemu wakati wa uhai wake amesema atamkumbuka Marehemu Danni Makanga kwa uchapakazi wake, huku akimwelezea kuwa wakati akiwa mbunge aliwahi kuwa mjumbe wa Baraza la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam ambapo alisaidia kutatua mambo mbalimbali kupitia chombo hicho cha maamuzi katika chuo.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa pole kwa familia, ndugu na marafiki wa marehemu Danni Makanga huku akisisitiza kuwa viongozi wa Chama na Serikali Mkoani humo wameonesha ushirikiano tangu walipopata taarifa za msiba mpaka wakati wa mazishi ili kumsindikiza marehemu aliyekuwa kiongozi katika heshima zote za Chama na Serikali.

Akitoa mahubiri wakati wa ibada ya mazishi, Padri wa Kigango cha Mtakatifu Michael Kidulya, Parokia ya Mtakatifu Luka Bariadi, James. Kitasanja amewaasa watu wote kujiandaa kwa kuwa hakuna ajuaye siku ya kufa kwake, huku akiwasisitiza kushika maagizo ya Mungu ikiwa ni pamoja na kuwapenda na kuishi vizuri na watu wote.

Marehemu Danni Makanga alifariki Juni 23 katika ajali iliyohusisha lori na pikipiki Mkoani Mwanza, ambapo wakati wa uhai wake aliwahi kuwa mbunge, mkuu wa wilaya na mpaka mauti inamkuta alikuwa Katibu wa Itikadi  na Uenezi wa CCM Mkoa wa Simiyu, ameacha mke na watoto watano.

MWISHO

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa