• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Maswa Yazindua Mfuko wa Walimu Kuwasaidia Kupata Mikopo Yenye Riba Nafuu Na Stella Kalinga, Simiyu

Posted on: November 29th, 2019

Wilaya ya Maswa imezindua mfuko wa walimu kwa lengo la kuwasaidia walimu ambao hawana sifa za kukopesheka katika taasisi zingine za fedha ili waweze kupata mikopo kwa riba nafuu.

Mfuko huo umezinduliwa na Katibu wa Chama cha Walimu nchini, Mwl. Deus Seif wakati wa hafla ya kuwapongeza walimu zaidi ya 1400 wa shule za msingi 123 za wilaya hiyo kwa kuwezesha wilaya kufanya vizuri kwenye Matokeo ya darasa la saba na kuongeza ufaulu  kutoka asilimia 34.9 mwaka 2013 hadi kufikia asilimia 88.73 mwaka 2019.

Akizungumza na mamia ya walimu walioshiriki katika uzinduzi huo, Seif amewaasa walimu kutambua thamani waliyopewa na viongozi wa wilaya na mkoa kwa kuendelea kuwajibika kwa uadilifu mkubwa.

“ Nitoe wito kwa walimu wenzangu ambao si waadilifu wabadilike, wale watoro waache utoro, ambao ni walevi wache ulevi wafundishe watoto; lakini wazazi na ninyi mtusaidie kuhimiza watoto wawe na mahudhurio mazuri shuleni ili walimu waweze kufanya kazi yao vizuri,” alisema Seif.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Maswa, Dkt. Fredrick Sagamiko amesema hadi sasa mfuko huo umeingiziwa kiasi cha shilingi milioni 15 na halmashauri na baadaye wadau kuongeza kiasi cha shilingi milioni 15 na kuufanya mfuko huo kuwa na jumla ya shilingi milioni 30.

Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Antony Mtaka amewataka walimu kuacha tabia ya kukopa fedha katika taasisi nyingine za fedha hususani za binafsi zenye riba kubwa ambazo huwalazimu kuweka kadi zao za benki kama rehani, huku akishauri Benki ya walimu kuja na huduma zinazojibu changamoto za walimu ikiwemo kutoa mikopo kwa riba nafuu

Kwa upande wake Katibu wa CWT ameipongeza Wilaya ya Maswa kwa kuona haja kuwapongeza walimu na ya kuwasaidia walimu kwa kutoa mikopo yenye riba nafuu kupitia mfuko huo, ambapo CWT pia imeunga mkono juhudi Wilaya kwa kuchangia kiasi cha shilingi milioni Nane (8).

Wilaya hiyo pia imetoa zawadi ya majiko ya gesi 101 kama zawadi kwa shule hizo ili kuwawezesha walimu kupata chai asubuhi wakiwa shuleni na kuwapunguza walimu muda wa kwenda kutafuta huduma hiyo nje ya maeneo ya shule.

Mkuu wa Wilaya ya Maswa, Dkt. Seif Shekalaghe amesema mwaka 2018 Wilaya ilitoa majiko ya gesi kwa  shule 20 zilizofanya vizuri hivyo, majiko hayo yanatolewa kwa shule 101 ambazo hazikupata awali, pamoja na zawadi ya majiko shule zilizofanya vizuri zimepewa fedha taslimu shilingi 500,000.

Katika uzinduzi huo pia ilifanyika harambee kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa nyumba nne za walimu ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kukabiliana na changamoto ya upungufu wa nyumba za walimu

MWISHO

 KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/11/maswa-yazindua-mfuko-wa-walimu.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa