• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Maonesho ya Nanenane Kitaifa 2019 Yataboreshwa Zaidi ya Mwaka 2018: RC Mara

Posted on: July 24th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Mhe. Adam Malima amesema Mikoa ya Simiyu, Mara na Shinyanga inayounda Kanda ya Nanenane ya Ziwa Mashariki imekusudia kuboresha zaidi maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019  ambayo yanafanyika kwa mara ya pili sasa katika kanda hii kwenye Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu.

Malima ameyasema hayo jana katika kikao maalum cha maandalizi cha Kanda hiyo kilichofanyika kwa lengo la kutathmini hali ya maandalizi ya maonesho hayo ambayo yanatarajia kuanza tarehe 29 Julai, 2019 na kuhitimishwa rasmi Agosti 08, 2019.

Amesema kanda imekusudia kuboresha upatikanaji wa huduma za maji, umeme na miundombinu mingine muhimu ikiwa ni pamoja na kuongeza majengo ya kudumu ili katika siku za usoni kanda ya Ziwa Mashariki iwe sehemu ya kudumu ya maonesho ya Kilimo Biashara.

“Mwaka huu tumekusudia kuboresha maonesho ya Nanenane Kitaifa kuliko mwaka jana 2018, tumekubaliana kuboresha upatikanaji wa huduma katika maeneo ya viwanja vua maonesho na pia  tunakusudia kuongeza upatikanaji wa majengo ya kudumu kwa sababu kwa kadri tunavyokwenda  tunatarajia hapa iwe ni sehemu ya Maonesho ya Kilimo Biashara kwa kanda hii” alisema

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka amesema Maonesho ya Nanenane mwaka 2019 yatakuwa na waoneshaji wengi wa teknolojia za kilimo kuliko miaka  iliyopia, hivyo akawahakikishia wananchi wote kuona teknolojia mbalimbali ikiwa ni pamoja na za upukuchuaji, utengenezaji wa chakula cha mifugo, ukataji majani ya mifugo, uvunaji na teknolojia nyingine nyingi.

Naye Mkurugenzi wa Maendeleo ya Mazao Wizara ya Kilimo, Bw. Nyasebwa Chinagu amesema moja ya jukumu la wizara hiyo katika Maonesho haya ni kuhakikisha kuwa teknolojia sahihi zilizopo zinaoneshwa katika Maonesho ya nanenane ili wakulima, wafugaji na wavuvi waweze kupata maarifa na teknolojia sahihi katika kuongeza tija katika uzalishaji.

Maonesho ya haya yanatarajiwa kufunguliwa rasmi na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan na viongozi wengine wa Kitaifa watakuwepo katika siku maalum, akiwepo Waziri Mkuu wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda na mgeni rasmi katika kilele cha maonesho haya anatarajiwa kuwa Rais wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Maonesho ya Nanenane Kitaifa yanafanyika kwa mara ya pili sasa mkoani Simiyu chini ya kauli Mbiu:-“KILIMO, MIFUGO NA UVUVI KATIKA UKUAJI WA UCHUMI WA NCHI” tangu Kanda ya Ziwa ilipogawanywa katika kanda mbili yaani, Kanda ya Ziwa Mashariki(Simiyu, Mara na Shinyanga) na Kanda ya Ziwa Magharibi(Mwanza, Geita na Kagera).

MWISHO

KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGNISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/07/maonesho-ya-nanenane-kitaifa-2019.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa