• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Manyanya Atoa Wito kwa Wananchi Kushiriki Maonesho ya Nanenane Kujifunza, Waongeze Tija kwenye Uzalishaji

Posted on: August 2nd, 2019

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhandisi. Stella Manyanya ametoa wito kwa wananchi kushiriki katika Maonesho ya Nanenane kwa lengo la kujifunza ili waongeze tija katika uzalishaji, huku akibainisha kuwa maonesho haya yameboreshwa, kwa wadau na Taasisi zinazotoa huduma kuongezeka na maonesho hayo kuwa sura ya kuwasaidia wananchi kubadilika.

Mhandisi Manyanya ameyasema hayo Agosti 02, 2019 kwenye Maonesho ya Nanenane Kitaifa mwaka 2019 yanayofanyika Kanda ya Ziwa Mashariki viwanja vya Nyakabindi Bariadi mkoani Simiyu.

“ Maonesho ya mwaka huu yamefana sana na kufana kwake hakupo katika namna mahema yalivyo, bali ushiriki wa waoneshaji, wakulima wenyewe na nimefurahi kuona baadhi ya mambo yanafanyika kwa vitendo kama uhimilishaji wa ng’ombe, ufugaji wa samaki, uwepo wa taasisi kama TBS, Wakala wa vipimo na vyama vya ushirika”

“ Mimi naona tumeboresha zaidi namna ya kufanya haya maonesho kwenda zaidi katika sura ya kuwagusa wananchi ili waweze kubadilika na kutumia huduma zinazohitajika, nipende kuwashawishi wananchi wengi zaidi wasikose kuja kujifunza kupitia maonesho haya, wanapojifunza wanaongeza tija katika maeneo yao” alisisitiza Mhandisi. Manyanya.

Aidha, amezihamasisha Halmashauri zote nchini kutenga maeneo kwa ajili ya ujenzi wa viwanda na uwekezaji mwingine ili wawekezaji wanapopatikana kusiwe na mlolongo mrefu  katika kupata ardhi na kupata vibali mbalimbali, huku akibainisha kuwa Serikali imeshaweka miundombinu wezeshi  kwa uwekezaji kama upatikanaji wa umeme.

Amesema sekta binafsi ndiyo injini ya ukuaji wa uchumi katika Taifa hasa kwenye eneo la biashara na viwanda huku akiongeza kuwa ni vyema maonesho hayo yakawa na kiu ya kufanya mambo yatakayoweza kurahihisha shughuli za kibiashara.

Awali Naibu Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema wananchi wengi wa Mkoa wa Simiyu wanajishughulisha na shughuli za kilimo hivyo ipo haja ya kuwepo kituo endelevu cha mafunzo ya kilimo ili wakulima waweze kupata mahala pa kujifunzia .

“Kutokana na kwamba wananchi wengi wa Mkoa wa Simiyu wanategemea sana hasa shughuli za kilimo ipo haja ya kuwepo kituo endelevu kwa ajili ya mafunzo kitachowasaidia wakulima kupata elimu kila siku kutokana na uhitaji wao”.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Mhe. Anthony Mtaka ametoa wito kwa wananchi na wajasiriamali wa mkoa wa Simiyu kutembelea Viwanja vya Nanenane kwa lengo la kujifunza kutoka kwa wenzao kutoka maeneo mbalimbali ya nchi yetu namna wanavyofanya shughuli zao na namna walivyofanikiwa.

MWISHO

 KUPATA PICHA ZAIDI FUNGUA KIUNGANISHI HIKI:-https://simiyuregion.blogspot.com/2019/08/manyanya-atoa-wito-kwa-wananchi.html

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa