• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali yaulizwayo |
    • Barua pepe |
Simiyu Region

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Simiyu

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dhamira na Dira
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti ya Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Health Service and SocialWelfare
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Seksheni ya Elimu
      • Huduma za Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uhasibu na Fedha
      • TEHAMA
      • Ununuzi na Ugavi
      • Huduma za Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
      • Strong
    • Vifungu vya Sheria
    • Fomu za Maombi
    • Taarifa
    • Hotuba
    • Taratibu
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Vyombo vya Habari
    • Habari
    • Video
    • Albamu ya Picha
    • Matukio yajayo
  • Miradi
    • Miradi iliyotekelezwa
    • Miradi Inayoendelea
  • Wilaya na Halmashauri
    • Wilaya
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Bariadi
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Busega
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Itilima
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Maswa
      • Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Meatu
    • Halmashauri
      • Halmashauri ya Wilaya ya Bariadi
      • Halmashauri ya Mji wa Bariadi
      • Halmashauri ya Wilaya ya Busega
      • Halmashauri ya Wilaya ya Itilima
      • Halmashauri ya Wilaya ya Maswa
      • Halmashauri ya Wilaya ya Meatu
  • Uwekezaji na Utalii
    • Fursa za Uwekezaji
    • Wanyamapori na Utalii

Manyanya Aridhishwa Maandalizi Maonesho ya SIDO Kitaifa Simiyu Atoa Wito kwa Wananchi Kushiriki

Posted on: October 22nd, 2018

Naibu Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Mhandisi. Stella Manyanya amesema ameridhishwa na Maandalizi ya Maonesho ya Viwanda Vidogo (SIDO) Kitaifa, yatakayofanyika kuanzia Oktoba 23-28, 2018 katika Viwanja vya Nyakabindi Bariadi Mkoani Simiyu na kutoa wito kwa wananchi kushiriki maonesho hayo, ili kujionea teknolojia na mashine rahisi zitumikazo kuongeza thamani bidhaa mbalimbali.

Mhandisi Manyanya amesema pamoja na kuwepo wa teknolojia na mashine, wajasiriamali kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini wameshawasili kwa ajili ya kuja kuonesha bidhaa mbalimbali wanazozalisha hivyo.

“Nitumie nafasi hii kuwapongeza viongozi wa Mkoa wa Simiyu kwa maandalizi mazuri nimeridhishwa na maandaizi na niwaombe wananchi waMkoa wa Simiyu na maeneo mengine kufika katika maonesho ya kwanza ya Kitaifa ya Viwanda Vidogo, kupata teknolojia na mashine rahisi tunazozitumia katika kuongeza thamani za bidhaa zetu hapa nchini” alisema

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Shirika la kuhudumia Viwanda Vidogo SIDO, Prof. Sylvester Mpanduji amesema wajasiriamali zaidi ya 1000 kutoka mikoa yote hapa nchini wnatarajia kushiriki maonesho haya,

Aidha, Profesa Mpanduji amesema ametoa wito kwa wananchi kwenda kuona teknolojia mbalimbali rahisi ambazo watazitumia kuanzisha viwanda, huku akibainisha kuwa shirika hilo litahakikisha viwanda vyote vinavyoanzishwa na Watanzania vinakuwa ili ifikapo mwaka 2025 nchi iwe na viwanda vikubwa vinavyoendeshwa na Watanzania.

Nao Wajasiriamali kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini wameeleza matumani yao kupitia Maonesho haya katika kuona teknolojia mpya katika utengenezaji wa bidhaa zao, kujifunza kutoka kwa wenzao na kuboresha bidhaa zao pamoja na kuongeza wigo wa masoko ya bidhaa zao.

“Haya ni maonesho ya kwanza kufanyika Kitaifa nina imani yatakuwa makubwa kuliko tulikuwa tukifanya awali, nina matumaini makubwa kuwa nitakutana na wajasiriamali wenzangu na kujifunza mengi kwao, kukutana na wananchi wa Simiyu na maeneo mengine nikauza bidhaa zangu zote zikaisha” alisema Hapyness Mabula kutoka mkoa wa Mwanza.

“ Katika maonesho haya natarajia kujifunza mambo mengi sana kwa sababu ni ya Kitaifa tofauti na yale tuliyokuwa tunaonana kikanda,naamini nitatanua wigo wa wajasiriamali nitakaokutana nao pamoja na soko la bidhaa zangu ninazozalisha” alisema Hamisi Samade kutoka mkoa wa Singida.

Katka hatua nyingine wajasiriamali hao wameomba Serikali iwasiadie katika upatikanaji wamitaji na kutatua changamoto zinazowakabili mipakani wanaposafirisha bidhaa zao wanazozalisha au malighafi zinazotumika katika uzalishaji wa bidhaa zao..

Maonesho ya SIDO Kitaifa yatafunguliwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa na yanatarajiwa kuhitimishwa na Rais wa Zanzibar Dkt. Ali Mohammed Shein.

MWISHO

Matangazo

  • Wanafunzi wa Mkoa wa Simiyu waliochaguliwa Kidato cha Kwanza mwaka 2021 Shule za Serikali za Bweni na Kutwa December 18, 2020
  • Karibu Mwenge wa Uhuru Mkoani Simiyu July 04, 2022
  • " Tuna zoezi la Senza Mbele yetuni tarehe 23 Agosti 2022 Binafsi nipo tayari kuhesabiwa, nawe ukihesabiwa, wore tutakuwa tumehesaniwa na mipango endelevu itapangwa Kwa ajili yeti. Sensa Kwa maendeleo jiandae kuhesabiwa" Mhe. David Kafulila July 08, 2022
  • Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa Kujiunga na Kidato cha Kwanza Mwaka 2020 - Chaguo la Pili (Second Selection) January 03, 2020
  • Fungua

Habari Mpya

  • DKT. YAHAYA ESMAIL NAWANDA MKUU WA MKOA MPYA SIMIYU

    July 28, 2022
  • RC. KAFULILA APIGA MARUFUKU USAFIRISHAJI ABIRIA KWA MAGARI MADOGO YANAYO TAMBULIKA KAMA "MCHOMOKO"

    July 13, 2022
  • WANAOWAKOPA WAKULIMA WA PAMBA KUKIONA-RC KAFULILA.

    July 09, 2022
  • Mwenge wa Uhuru Umewasili Mkoani Simiyu

    July 06, 2022
  • Fungua

Video

Upimaji wa maeneo ya wakulima na wafugaji kupitia Teknolojia ya Ndege Nyuki (Drones)
Video Nyingine

Kurasa za Karibu

  • Mwongozo wa Uwekezaji wa Mkoa(Fursa za Uwekezaji)
  • Historia ya Mkoa
  • Takwimu za haraka
  • Picha za Matukio Mbalimbali
  • Vivutio vya Utalii

Kurasa Mashuhuri

  • Tovuti ya Ikulu
  • TAMISEMI
  • Utumishi
  • Tovuti ya Ajira
  • Tovuti ya Serikali
  • Watumishi Portal

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

free HitCounter

Ramani ya Eneo

Wasiliana nasi

    Bariadi - Somanda

    Anuani ya Posta: S. L. P. 4, BARIADI.

    Simu ya Mezani: 028-2700011/2700054

    Simu ya Mkononi: 028-2700011/2700054

    Barua Pepe: ras@simiyu.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali yaulizwayo
    • Ramani

Hati Miliki ©2017 Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Simiyu.Haki Zote Zimehifadhiwa